NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Thursday, January 31, 2013

TAARIFA ZA MSIBA ALIOPATA MSANII SUMALEE JAN 31 2013 PAMOJA NA ZA MATATIZO YA PASSPORT YAKE UK


Sumalee akiwa Uingereza ambako alikwenda toka december 2012 akiwa na Barnaba.
Miezi 8 toka mama yake mzazi afariki dunia, msanii wa bongofleva Sumalee amepata pigo jingine baada ya baba yake mzazi kufariki january 31 2013.
Taarifa zilizoifikia the hood's pick ni kwamba baba yake alifariki jana jioni wakati bado Sumalee yuko Uingereza kwa shughuli za kimuziki.
Kwenye Exclusive interview na the hood's pick december 12 2012 Suma alisema mambo mawili yaliyomuhuzunisha sana 2012 ni kuibiwa gari lake pamoja na kufiwa na mama yake mzazi mwezi April.
Namkariri akisema “mama yangu amekufa kwenye mikono yangu, yuko kwenye mapaja yangu na mikononi nilikua namsomea dua tu”
Kulikua kuna taarifa kwamba Sumalee kapata matatizo ya hati yake ya kusafiria huko Uingereza hivyo itakua ngumu kuja Tanzania msibani lakini taarifa nilizonazo kutoka kwa mtu wa karibu ni kwamba hajapata tatizo lolote kama wengi wanavyodhani, kilichotokea ni kwamba alitaka kuongeza miezi sita ya kuendelea kukaa Uingereza hivyo ikabidi Passport aiache ubalozini ambapo ghafla ndio akapata msiba hivyo itabidi asafiri kwa kutumia documents.
Mtu huyu wa karibu wa Sumalee ameiambia millardayo.com kwamba baba mzazi wa Sumalee anazikwa leo february 1 2013 na Sumalee wamejaribu kuwasiliana nae hapatikani kwenye simu hivyo hakuna uhakika kama yuko kwenye ndege kuja Tanzania ama la.
the hood's pick inatoa pole kwa Sumalee, familia na ndugu kwa msiba huu.

MAMA AUZA GARI LA SHARO, AFUNGUKIA...

Na Gladness Mallya
MAMA wa aliyekuwa msanii wa muziki na filamu Bongo, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ amefungukia gari aliloacha mwanaye pamoja na mimba ambayo inadaiwa ni yake.
Gari aina ya Toyota Opa aliyoiacha marehemu Sharo Milionea.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Mama Sharo alisema: “Kuhusu gari lile Toyota Opa aliloacha marehemu mwanangu naliuza kwani siwezi kuliendesha na haliwezi kukaa bila kufanya kazi yoyote.
“Kwa upande wa Marry Lucas wa Sumbawanga msichana aliyejitokeza baada ya Sharo kufariki na kusema ana ujauzito wake, siwezi kumtambua kwa sababu enzi za uhai Sharo hakuniambia kuwa ana mchumba wala mpenzi.”
Sharo Milionea alifariki dunia Nov 26, mwaka jana kwa ajali ya gari iliyotokea mkoani Tanga.
Siku chache baadaye, Marry aliibuka na kudai alikuwa mpenzi wa Sharo na ana ujauzito wake.

MCHUNGAJI ADAIWA KUMUACHA MKEWE KWA USHIRIKINA

Na Mwandishi Wetu
MCHUNGAJI wa Kanisa la Calnel Centre lililopo Uwanja Ndege mjini hapa, Elias Ambakisye (pichani juu) amemuacha mkewe aitwaye Sabina Lameck kwa madai ya ushirikina.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni katika kikao kilichohudhuriwa na familia ya mchungaji huyo, wazee wa kanisa na waandishi wa habari kilichoitishwa na mtumishi huyo wa Mungu.
Habari zaidi kutoka kwa chanzo chetu zinapasha kwamba, mchungaji huyo aliitisha kikao hicho ili wahudhuriaji wamsikie Sabina aliyekuwa mkewe kabla ya kuachana miaka minne iliyopita akitubu mambo ya kishirikina aliyomtendea.
Imedaiwa kuwa, baada ya mama huyo kupewa nafasi ya kutubu alianza kumtuhumu muumini wa kanisa hilo (jina kapuni) kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Ambakisye ambaye ni mumewe wa ndoa.
Habari zinaongeza kuwa, Sabina aliwaeleza wahudhuriaji wa kikao hicho kwamba mwanamke huyo alichukua nguo za mchungaji na za kwake na kuzipeleka kwa kalumanzila zikafanyiwe ndumba ili warudiane na mumewe.
Sabina aliongeza kuwa, jambo la kushangaza ni kwamba baada ya kufanya ushirikina hawajarudiana na mumewe isipokuwa imekuwa kinyume kwani Ambakisye anataka kumuoa muumini huyo.
Kwa upande wake mchungaji huyo, alimtuhumu Sabina kwamba ni mshirikina na kudai aliamua kutengana naye kutokana na tabia hiyo pia kuzaa na mwanaume mwingine kitendo kilichomdhalilisha sana.

SOO LA BASTOLA, TUNDA MAN AKIONA CHA MOTO

Na Shakoor Jongo
TABIA ya baadhi ya mastaa kuonyeshaonyesha bastola hadharani kimemtokea puani ‘memba’ wa Kundi la Tip Top Connection, Khalid Ramadhani ‘Tunda Man’ baada ya hivi karibuni kuitwa na jeshi la polisi na kuhenyeshwa.
 

Khalid Ramadhani ‘Tunda Man’.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni Tunda Man alisema makala iliyotoka kwenye gazeti ndugu na hili la Ijumaa Wikienda ikieleza jinsi baadhi ya wasanii wanavyozianika silaha kiholela imemfanya akione cha moto kwani wakati akizungumza na mwandishi wetu alikuwa Kituo cha Polisi cha Kati (Central) akihojiwa.
“Kwanza naomba nikwambie kuwa hakuna kitu ambacho kimenikosesha amani leo (Jumatatu) kama hii habari yako uliyoandika kwenye gazeti, hivi ninavyoongea na wewe niko ‘sentro’ nikihojiwa, kiukweli sina amani,” alisema Tunda Man.
Hivi karibuni msanii wa muziki, Aboubakar Chende ‘Dogo Janja’ alinaswa akiwa na bastola na alipoulizwa ni ya nani alidai ni ya Tunda Man hivyo kumpa msala mwenzake.

DK. CHENI: NIMEMALIZA KWA LULU NAHAMIA KWA KAJALA


Na Gladness Mallya
STAA aliyekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha msanii wa filamu Elizabeth Michael ‘Lulu’ anapata dhamana, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ amefunguka kuwa baada ya kufanikiwa kwa Lulu sasa anahamia kwa msanii mwingine, Kajala Masanja.     
Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ akiwa na Lulu pamoja na mama yake baada ya kukamilisha dhamana.
Akizungumza nje ya Mahakama Kuu jijini Dar baada ya Lulu kuachiwa, Dk. Cheni alisema kwa sasa anaanza mchakato wa kumsaidia Kajala mpaka ajue hatima ya kesi  inayomkabili.
“Unajua Lulu siyo mtu wa kwanza kumsaidia na mama yake ndiye aliniomba, nilishawasaidia wengi. Hata Cloud alipofungwa nilifuatilia mimi na Dude mpaka mwisho, hatukukata tamaa na kwa Kajala nitafanya hivyo kwa sababu ni mwenzetu jamani, naamini Mungu anaweza sana na atafanikisha kila kitu,” alisema Dk. Cheni.
Kajala anasota Segerea akikabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyokuwa imewekwa bondi na serikali kutokana na mumewe kutakatisha fedha haramu.

HIZI NI KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI 16 YA LEO FEB 1 2013.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Tuesday, January 29, 2013

KUMBE CHANZO UCHAWI, TRAFIKI

Stori:  Mwandishi Wetu, Masasi
KILA kinachotajwa kusababisha vurugu za Mtwara ni gesi lakini Uwazi lina vitu ambavyo vimekuwa havitajwi katika sakata hilo.
Uchunguzi uliofanywa na ripota wetu, umebaini kuwa imani za kishirikina na tukio la trafiki aliyemgonga mwendesha bodaboda na kumvunja mguu, ndiyo asili ya vurugu hizo.
TRAFIKI MASASI
Habari kutoka chanzo chetu wilayani Masasi zinasema, kilichosababisha vurugu ni askari wa usalama barabarani aliyemgonga dereva wa bodaboda na kumvunja mguu kisha polisi wa Kituo cha Polisi cha Sokoni kukataa kutoa PF 3 ili majeruhi akatibiwe.
Chanzo chetu kilisema, baada ya tukio hilo, madereva wa bodaboda waliungana na wa bajaj kwenda kwa kamanda wa polisi wa wilaya lakini hawakuruhusiwa kumuona.
“Hasira za mwenzao kunyimwa PF3 pamoja  na kukataliwa kumuona OCD, vilisababisha maandamano na uharibifu wa mali.
“Katikati ya maandamano ndipo watu hao wakaibuka kudai haki kwa jumla, ikiwemo gesi kutosafirishwa kutoka Mtwara. Kabla ya hapo Masasi hakukuwahi kuwa na maandamano ya kupinga gesi kusafirishwa,” kilisema chanzo chetu.
UHARIBIFU WA MALI MASASI
Mali zilizoharibiwa ni pamoja na nyumba za wabunge, Mariam Kasembe (Masasi Mjini), Anna Abdallah (Viti Maalum), majengo ya Mahakama ya Mwanzo, Ofisi ya CCM ya Wilaya, Ofisi za Halmashauri ya Wilaya, Kituo cha Polisi Sokoni na magari 12.
Nyumba ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa haikosogelewa kutokana na ulinzi mkali uliowekwa na polisi japokuwa haipo mbali na ofisi zilizounguzwa na waandamanaji.
“Kweli gesi ilitajwa lakini ni suala lililoibuka baadaye, ukweli ni kwamba chanzo chake hasa ni yule trafiki aliyemfukuza dereva wa bodaboda akamgonga, akasababisha aanguke na kutumbukia mtaroni na kuvunjika mguu. Aliponyimwa PF3 ndipo vurugu zilipoanza,” kilisema chanzo chetu.
MTWARA NA UCHAWI
Kata ya Chikongola, Manispaa ya Mtwara Mikindani, wananchi waliizingira nyumba ya diwani wa kata hiyo, Mohammedi Chehako kwa madai ya kuwahifadhi wachawi ndani ya nyumba yake.
Chanzo chetu kilieleza: “Wananchi walikuta ungo ukiwa na tunguri ndani, wakadai ile ni ndege ya wachawi ambayo huitumia kusafiria angani.
“Wananchi walidai ule ungo na tunguri, maana yake wachawi wamedondoka, wakadai watakuwa wamehifadhiwa kwenye nyumba ya diwani huyo.
“Diwani kukata mzizi wa fitina, aliuchoma moto ule ungo pamoja na tunguri lililokuwemo lakini wananchi waliendelea kusisitiza wapewe wachawi waliodondoka na ungo na kuhifadhiwa ndani ya nyumba ya diwani.
“Kadiri muda ulivyosogea ndivyo na watu walivyoongezeka, hali ikawa mbaya nyumbani kwa diwani, kwa hiyo Diwani Chehako akapiga simu polisi kuomba msaada.
“Polisi walipofika pale nyumbani kwa diwani waliwasihi wananchi kutawanyika kwa kuwa ungo na tunguri vilishachomwa moto mbele yao.
Chanzo chetu kiliendelea kusema: “Badala ya kutii walichoambiwa na polisi, wananchi hao walianza kurusha mawe na ndipo polisi walipojibu kwa kupiga mabomu ya machozi.
“Yale mabomu ya machozi yakaibua vurugu kubwa, kwa hasira wananchi wa Mtwara wakaamua kukumbushia na sakata la gesi, maandamano yakawa makubwa zaidi, lakini ukweli chanzo chake ni ule ungo na tunguri nyumbani kwa diwani.”
DIWANI ANENA
Akisimulia mkasa huo, Diwani Chehako alibainisha kuwa ni kawaida yake kuamka alfajiri kwa ajili ya sala ya asubuhi, lakini asubuhi ya tukio alishindwa kufanya hivyo, japo hakuhisi chochote.
“Ilipofika saa 12 asubuhi nikaanza kusikia watu wakishangaa kitu nje ya nyumba yangu, nilipotoka nikakuta ungo na tunguri ndani yake. Mara wakaja vijana wawili na pikipiki wakachukua ule ungo na kukimbia nao.
“Nikawatuma vijana wawafuate waurudishe, walifanikiwa na ungo ule ulirejeshwa nyumbani hapa na ndipo nilipouteketeza kwa moto, ” alisema.
Akaongeza: “Nilidhani yatakuwa yameisha, lakini wananchi waliendelea kudai nimewafungia wahusika ndani wakati si kweli, ndipo nilipowaita polisi na baada ya kukataa amri ya kutawanyika, walichaguliwa wananchi watano kukagua ndani kama kuna wachawi, hawakuwaona ndipo  wakaanza kurusha mawe na vurugu zikaanza.
“Wananchi hao wenye vurugu hawakuishia hapo, wakavamia mahakama ya mwanzo kwa kupiga mawe jengo hilo na kuvuja vioo kisha kuchoma moto matenki ya maji.
“Ilibidi polisi wafanye kazi ya ziada ya kuondoa majalada yote yaliyokuwa ndani ya mahakama hiyo.
“Vurugu zilipamba moto baada ya vijana hao kuanza kuimba, ‘Tunataka gesi yetu’, hivyo kuonekana wazi kuwa wapo walioingia katika vurugu kwa kufuata mkumbo bila kujua chanzo wakafanya maandamano ya hasira kudai gesi.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Maria Nzuki alisema gari moja la polisi lenye namba PT 1421 limevunjwa kioo cha mbele kwa mawe.
Hata hivyo, hakutaka kuzungumza zaidi badala yake alisema kwa kifupi: “Ndugu mwandishi hali halisi unajionea mwenyewe wala sina cha kuongea.”

JE, NI KWELI CHAI INAPUNGUZA HATARI YA MTU KUPATWA NA UGONJWA WA MOYO?



CHAI imeanza kutumiwa nchini China zaidi ya miaka 4,000 iliyopita na kwa mujibu wa historia, Mtawala Shen-Nung, katika miaka ya 2737 BC, ndiye aliyekuwa akinywa chai kwa staili ya kunywa maji ya moto ambayo yaliangukiwa kwa bahati mbaya na majani ya chai. Kuanzia wakati huo unywaji chai ulindelea kukua na kusambaa duniani kama ilivyo leo.
Kabla ya kujibu swali la makala yetu ya leo, kuna umuhimu wa kuifahama chai kwanza. Kuna aina mbili za chai- Kijani na Nyeusi (Green & Black tea), ambazo utayarishaji wake unatofautiana. Chai ya kijani hupashwa joto mara baada ya kuchumwa na haifanyiwi mchakato mwingine.
Wakati chai nyeusi hukaushwa mara baada ya kuchumwa na huachwa ipate hewa kabla ya kupashwa joto. Matokeo yake chai ya kijani na nyeusi hutofautiana hata kwa muonekano, ladha na kemikali zilizomo ndani yake. Chai ya kijani inapendwa sana katika bara la Asia wakati chai nyeusi hupendelewa zaidi katika nchi za magharibi.
Aina zote mbili za chai zina kitu kinachoitwa ‘caffeine’, dawa ambayo ina athari ya kiwango fulani katika uchangamfu wa mwili. Kiwango cha ‘caffeine’ kinachopatikana kwa kunywa kikombe kimoja cha chai, kinategemea na wingi wa chai iliyowekwa, kikombe kilichowekwa chai nyingi (strong tea) kitakuwa na kiwango kikubwa cha ‘caffeine’ tofauti na kile kilichowekwa kiasi kidogo cha chai.
Ingawa haijathibitika kisayansi kama ‘caffeine’ haina madhara kabisa kwa mtoto aliye tumboni, inashauriwa kuwa wanawake wajawazito na akina mama wanaonyonyesha, wasinywe kiwango kubwa cha ‘caffeine’, hii ina maana kwamba unywaji wao wa chai uwe ni kwa kiwango kidogo, kikombe kimoja cha chai nyepesi kwa siku.
 
CHAI NA UGONJWA WA MOYO, SARATANI
Kwa miaka mingi sasa, imekuwa ikidhaniwa kuwa unywaji wa chai unaweza kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa moyo. Chai inaweza kutoa kinga dhidi ya ugonjwa huo kupitia virutubisho vyenye uwezo wa kudhibiti kuganda kwa damu mwilini, kitaalamu vinajulikana kama ‘antioxidants’ ambavyo vimo kwenye chai. Virutubisho hivyo pia vina uwezo wa kupunguza hatari ya mtu kupatwa na saratani.
Kwa mujibu wa watafiti mbalimbali duniani, ushahidi uliyopo kuhusu chai, ingawa siyo mkubwa sana, unaonesha kuwa chai ina manufaa kwa ujumla kiafya, na hasa kwa moyo. Utafiti mwingi umeonesha kuwa watu wanaokunywa chai wako katika hatari ndogo ya kupatwa na ugonjwa wa moyo kuliko wasiokunywa chai.
Bila shaka, kunaweza kuwepo na sababu nyingine zinazowafanya wanywaji chai kuwa salama. Aidha ushahidi wa kwenye maabara umethibitisha kuwa virutubisho vilivyomo kwenye chai hupunguza kasi ya kuganda kwa damu kwenye mishipa ambako hatimaye husababisha ugonjwa wa moyo na hatimaye kiharusi.
Swali moja ambalo bado halijapatiwa majibu sahihi ni iwapo kuongeza maziwa kwenye chai kuna athari yoyote kiafya. Utafiti wa awali ulionesha kuwa maziwa yanaweza kuingilia uwezo wa chai wa kuipa damu kinga, lakini utafiti wa hivi karibuni umebaini kuwa maziwa hayawezi kuingilia uwezo wa virutubisho (antioxidants) vilivyomo kwenye chai kufanya kazi yake ya kulinda damu isigande. Hivyo chai na maziwa nayo ni salama tu.
Jambo la kuzingatia ni kwamba unjwaji wa chai pamoja na chakula huingiliana na upatikanaji wa madini ya chuma mwilini yanayopatikana kwenye vyakula vitokanavyo na mimea.
Watu wenye madini chuma mengi mwilini (hali inayojulikana kitaalamu kama ‘haemochromatosis), ndiyo wanaoruhusiwa kula chakula huku wakinywa na chai. Hata hivyo kiwango chako cha madini ya chuma mwilini kitakuwa kizuri iwapo utakunywa chai kati ya mlo badala ya kunywa na chakula.
Jambo lingine la kuzingatia katika unywaji wa chai ni kiwango, kwani kiwango kitakachokupa faida zilizoelezwa hapa ni kile kisichozidi kikombe kimoja kwa siku, kiwango kikizidi  sana husababisha matatizo mengine, ikiwemo suala la ukosefu wa choo (constipation).

MAPENZI HUWA IMARA PALE YANAPOJENGEWA NJIA YA KUTOKA NA KUINGIA-4






MAISHA yakaendelea, Khalid hakuwa mtu mwenye pesa nyingi lakini aliamua kutumia akiba yake kuhakikisha Gift anakuwa na furaha, anatimiza pia ndoto zake. Khalid alieleza ombi lake la kumtaka wawe na uhusiano wa kimapenzi na panapo majaliwa, waweze kufunga ndoa.
Gift ombi hilo alilikubali. Wiki moja baadaye, Khalid alimsafirisha Gift kwa ndege kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kufuatilia nafasi za kujiunga na Chuo Kikuu cha Tiba Muhimbili. Hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa Gift kusafiri kwa ndege, aliona ndoto, akamshukuru sana Khalid.
Alipata chuo, Khalid akamlipia ada, bweni na matumizi mengine. Kwa kifupi Khalid aligeuka baba kwa Gift, alimhudumia kila kitu. Gift alipopatwa na tatizo lolote, mtu wa kwanza kumpigia alikuwa ni Khalid ambaye alitatua bila kusita, akijua anajenga maisha ya mkewe mtarajiwa.
Kuna wakati ubinadamu ulimuingia Khalid, akawa anaomba kufanya mapenzi na Gift lakini hakufanikiwa. Siku zote Gift alimwambia asubiri mpaka watakapofunga ndoa. Japo Khalid ilimuuma lakini upande mwingine aliona msimamo wa Gift ni mzuri na alilegea kila alipokumbuka kauli tamu ya Gift: “Usijali mpenzi wangu, mimi ni wako, tutafanya mpaka utachoka.”
Siku, wiki, miezi, ikawa mwaka, miaka ikapita, Gift akamaliza chuo. Hakutaka hata kurudi Mwanza. Alichokikataa ni kuonana na Khalid. Alimuona mwanaume asiye na elimu, kwa hiyo kuwa na mume aina yake aliona kama ni kupoteza dira ya maisha. Wanaume wasomi ni wengi.
Khalid alijitahidi kufika Dar es Salaam, akaa mwezi mzima bila kuonana na Gift ambaye kwa kuona kero, akaamua kubadili na namba ya simu. Kutokana na uhusiano wao kutambuliwa mpaka na wazazi pamoja na ndugu wengine, aliwashirikisha lakini hakuna alichoambulia.
Sabrina ni rafiki yake Gift, akaamua kuingilia kati, kumshauri Gift atambue umuhimu wa Khalid kwa sababu pale alipo asingefika kama siyo mwanaume huyo lakini ushauri huo ulionekana sawa na takataka: “Sikiliza Sabrina, mimi ni msomi, daktari, natakiwa niwe na mwanaume msomi mwenzangu.”
Akaendelea: “Nilikuwa na Khalid kwa sababu alijipendekeza kwangu na alionesha anao uwezo wa kunisaidia. Nisingeweza kuacha hiyo nafasi lakini sasa hivi nimefanikiwa, Khalid kwangu wa nini tena? Ataniharibia tu maisha yangu. Lazima niyatengeneze maisha yangu kisomi.”
Gift alipoona msimamo wa Sabrina kwa Khalid umekuwa mkali, akimsisitiza anachokifanya siyo kizuri, alimjibu: “Hivi Sabrina, na wewe si mwanamke? Kama unamuona Khalid ni mwanaume wa maana sana, si uende akakuoe wewe? Tusisumbuane, kwanza yule siyo mwanaume wangu, sijawahi kutembea naye.”
Khalid alilia, machozi yakakauka, akaamua kuongeza juhudi kwenye biashara zake. Hatua zilikuwa ndefu na mafanikio yaliendelea kwa Khalid. Akafanikiwa kuanzisha maduka ya nguo, Dar es Salaam, Mwanza na Arusha. Vilevile akaanzisha biashara mbalimbali ambazo zilimfanya kuwa anasafiri kwenda nchi mbalimbali.
Kutokana na historia yake ya kukosa mke kwa sababu ya elimu, aliamua kutumia utajiri wake kuanzisha mfuko kwa ajili ya kuwasaidia vijana wa kiume kujiendeleza kielimu. Alifanya mambo mengi makubwa, ikiwemo kujenga majumba ambayo baadhi aliyafanya kuwa ofisi zake kwa ajili ya kuratibu biashara zake.
Khalid alipotaka kufunga ndoa, akamuona Sabrina ndiyo mke sahihi kwake. Japo mwanzoni ilikuwa ngumu kueleweka lakini baadaye kilieleweka. Gift aliposikia Sabrina na Khalid wamefunga ndoa, moyo ukamuuma sana, aliumia zaidi kwa sababu wanaume wasomi aliowataka walimtesa sana.
Hata hivyo, hiyo haikumuuma kama siku alipoomba kazi kwenye hospitali binafsi inayoitwa KS Health Centre bila kujua inamilikiwa na nani. Siku anaitwa kwenye usaili ndipo aliposhtuka, kugundua kwamba hospitali hiyo ni ya Khalid lakini inasimamiwa na mkewe (Sabrina) ambaye naye ni daktari.
Gift baada ya kufanyiwa usaili, aliondoka kichwa kikiwa kizito. Wakati yeye alikwenda kwenye usaili akiwa na taksi na kuondoka kwa taksi, kwa macho yake alimshuhudia Sabrina anaendesha gari la kifahari aina ya BMW X6 rangi ya chungwa.
Kwa haraka, Gift akaingiwa na mawazo kwamba kumbe maisha ya raha aliyonayo Sabrina, yangekuwa yake kama asingemdharau Khalid. Alimuona ni kijana aliyeishia kidato cha nne lakini ameweza kufanya mambo makubwa kumuwezesha kumiliki pesa na mali nyingi.
Mfano wangu una maana kuwa Gift ni mnyonyaji, alimuona Khalid ni daraja la kutimiza malengo yake kimaisha bila kuzingatia kwamba Khalid naye ni binadam. Kumbe badala ya kumfanyia visa, kumnynyasa, kumsimanga na kumdhalilisha kielimu, angeweza kushirikiana naye kujenga maisha bora.
Ingependeza kama Gift angeona umuhimu wa kutumia elimu yake kushirikiana na Khalid kujenga maisha lakini kwa sababu aliingiwa na ubinafsi, dharau kwa kumuona ni mwaume mbumbumbu, ndiyo maana baadaye akajuta. Ni sawa na mtu anayekumbuka almasi aliyoitupa, wakati akiwa bize anakusanya mawe.
Hakuna sababu ya kujuta baadaye, wala haitakiwa kuachana kisa mmoja amemuona mwenzake mnyonyaji, isipokuwa kila mmoja anapaswa kujiuliza na kupata jibu: “Ninapewa, je mimi natoa nini kwa mwenzangu?”


MAITI YA KICHANGA YAGEUKA JOGOO


Stori: Makongoro Oging’
BADO tupo mwanzoni mwa mwaka lakini tukio la maiti ya kichanga kugeuka jogoo ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es Salaam linaweza kuongoza mengine yote ya ajabu yanayoweza kujiri ndani ya 2013.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela.
Mwananyama ni hospitali yenye hadhi ya mkoa kitabibu, ina rekodi za kuwa na matukio ya ajabu, ila hili siyo tu kwamba linaingia miongoni mwa hayo bali pia linaweza kutia fora.
Asubuhi ya Jumatano iliyopita, ilikuwa kizaazaa pale jokofu lililotumika kuhifadhi maiti ya kichanga cha mtoto, kukutwa kuna jogoo.
Mshangao zaidi ni kwamba ndani ya lile jokofu, pembeni ya yule jogoo, kulikuwa na hirizi pamoja na tunguri.
TUKIO LILIKUWA HIVI
Habari kutoka vyanzo vyetu, zimewekwa wazi kuwa Jumanne iliyopita, saa 7 mchana, polisi walipigiwa simu, wakataarifiwa kuhusu maiti ya mtoto iliyokuwa imetelekezwa eneo la Kigogo, Mbuyuni, Dar es Salaam.
Vyanzo vyetu vimebainisha kuwa polisi baada ya kupata taarifa hizo walifika eneo la tukio na kukuta maiti hiyo ya kichanga ikiwa imefunikwa kwa kuzungushiwa sanda.
ETI, KILIKUWA KICHANGA CHA KIKE
Kwa mujibu wa Moses Madilu, mkazi wa Kigogo, aliyedai kushuhudia tukio hilo, polisi walipofika eneo la tukio waliikagua maiti hiyo na kubaini kwamba ni ya kike.
Chanzo chetu kikaeleza kuwa baadhi ya mashuhuda, hususan wanawake, walitokwa na machozi kwa masikitiko kwamba itakuwa mtu alijifungua halafu akakinyonga kichanga hicho kabla ya kukitelekeza eneo hilo.
“Baada ya kujiridhisha kwa kazi yao, polisi waliichukua maiti hiyo ya kichanga, wakaipakia kwenye ‘difenda’, wakaipeleka Hospitali ya Mwananyamala,” kilieleza chanzo chetu.
HOSPITALI YA MWANANYAMALA
Ndani ya hospitali hiyo, mwandishi wetu alielezwa kuwa polisi walipofika, walishusha maiti hiyo na kumkabidhi mganga wa zamu aliyejulikana kwa jina moja la Dk. Liwa.
Muuguzi mmoja wa hospitali hiyo (jina tunalo) alisema: “Dk. Liwa aliwaambia wale polisi wapeleke maiti hiyo mochwari.
“Polisi walifanya hivyo lakini kule mochwari walimkuta msimamizi mkuu, Omar Buyoya aliyekataa kuipokea kwa vile daktari hakuthibitisha kama kile kichanga kilikufa au kilikuwa hai.
“Polisi na Buyoya walivutana kwa muda mrefu, alitokea mhudumu mwingine wa mochwari aliyekuwa akijuana na polisi mmoja aliyebeba ile maiti, alikubali kuupokea mwili huo na kuingiza ndani kwenye jokofu la kuhifadhia maiti.”
Muuguzi huyo aliendelea kusema kuwa siku iliyofuata, Dk. Liwa alifika mochwari na alipofungua jokofu na kufunua sanda, badala ya kukuta maiti ya kichanga, alikuta jogoo, tunguri na hirizi.
Dk.Liwa alipatwa  na mshangao mkubwa huku jasho likimtoka kutokana na uoga, aliwaita wafanyakazi ambao walijazana hapo  mochwari kushuhudia.
“Baadhi ya wafanyakazi walipigwa na butwaa huku wengine wakicheka hadi kudondoka chini na wakawa wanajiuliza kama kweli polisi wanaweza kupeleka jogoo hospitali au ni mambo ya kishirikina,” alisema muuguzi huyo.
Dk. Liwa na wafanyakazi wenzake waliondoka mochwari na kuacha hilo jogoo katika chumba cha maiti huku wakishindwa la kufanya.
MGANGA MKUU ANENA
Gazeti hili lilimtafuta Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk. Sophinias Ngonyani ambaye alikiri  kuonekana kwa jogoo badala ya maiti ya kichanga.
“Polisi walituletea kifurushi wakiamini kuwa ni maiti ya kitoto kichanga ambapo tulikipokea lakini ilipotazamwa na daktari, tulikuta jogoo, hirizi na tunguri, tuliamua kumchoma moto kwa sababu kile ni chumba cha kuhifadhi maiti siyo cha kuhifadhia mizoga ya kuku, ng’ombe au mbwa,” alisema Dk. Ngonyani.
POLISI WANENA
Naye Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, ACP Charles Kenyela alipoulizwa juu ya sakata hilo alisema kwamba wao kama jeshi la polisi walipigiwa simu na raia mwema kuwa  kuna maiti ya kichanga ambapo askari waliondoka hadi eneo la tukio na kuichukua mpaka Hospitali ya Mwananyamala.
“Polisi waliichukua hadi Hospitali ya Mwananyamala kwa wataalamu na baada ya kuikabidhi waliondoka na kuendelea na shughuli nyingine, nami nashangaa kusikia kwamba madaktari walikuta bonge la jogoo,” alisema Kenyela.
MASWALI MATANO
Je, ni kweli polisi waliikagua maiti na kugundua ni kichanga cha kike?
Kama ndiyo, ilikuwaje kikageuka jogoo?
Kwa nini daktari hakuipima ile maiti, badala yake akaelekeza ipelekwe mochwari?
Je, au polisi walibeba mzoga wa jogoo, wakampakia kwenye difenda wakidhani ni maiti ya kichanga?
Mkweli nani, polisi wanaodai kupeleka maiti ya kichanga, au hospitali wanaosema walipelekewa mzoga wa kuku, tunguri na hirizi?

Wanajeshi waudhibiti mji wa Timbuktu


 29 Januari, 2013 - Saa 07:30 GMC
Ndege za vikosi vya Ufanransa
Vikosi vya majeshi vinavyoongozwa na ufaransa kaskazini mwa Mali vimeudhibiti mji wa Timbuktu katika harakati za kukomboa eneo la kaskazini mwa Mali kutoka mikono ya wanamgambo wa kiislamu wanaohusishwa na kundi la kigaidi la Alqaeda.
Makamanda wa jeshi la Ufaransa wanasema kuwa wanajeshi wanashika doria kwenye barabara za miji wakilenga kuwafurusha wapiganaji waliosalia.
Pindi mji wa Timbuktu utakapokombolewa, wanajeshi wanatarajiwa kulenga kuwaondoa waasi katika eneo ambalo linakaliwa na waasi la na ngome yao Kidal.
Wakati huo huo mkutano wa wafadhili wa Mali unatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Ethiopia -Adis Ababa hii leo kuchangisha pesa kwa ajili vikosi vya kimataifa vinavyopigana dhidi ya waasi wa Kiislam.
Gharama za kuendesha harakati za kijeshi nchini Mali zinakadiriwa kuwa kati ya dolla milioni mia tano na dola bilioni moja .
Huku ahadi za misaada zilizotolewa hadi sasa na Mataifa ya Afrika na muungano wa ulaya zikiwa ni dola milioni moja, zaidi ya wahisani sitini walioalikwa katika mkutano huo wanatarajiwa kuziba pengo hilo.
Na Mkutano mwingine unafanyika mjini Brassels kuamua juu ya kutumwa kwa kikosi cha muungano wa ulaya cha kutoa mafunzo kwa askari wa serikali ya mali.
Wapiganaji nje ya  mji wa Timbuktu
Tayari Uingereza itatoa wakufunzi kwa ajili ya mpango huo.
Muungabno wa Ulaya ambao umekalimisha mkutano wake mjini humo, unatumai kuwa kongamano hilo litaweza kuchangisha pesa za kikosi cha pamoja kukabiliana na waasio hao.
Wanajeshi wa Ufaransa, nchini Mali, siku ya Jumatatu, waliweza kudhibiti uwanja wa ndege katika mji muhimu wa Timbuktu.
Kwa mujibu wa afisaa majeshi hayo, waliudhubiti mji huo bila upinzani kutoka kwa wapiganaji wa kiisilamu.
Wanajeshi wa Mali na Ufaransa, wamekuwa wakipigana kuelezea Kaskazini mwa nchi dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu.
Siku ya Jumamosi , waliuteka mji wa Gao, mji wenye idadi kubwa ya watu nchini Mali.
Maelfu ya watu walikusanyika kwenye barabara za mji kusherehekea kuwasili kwa wanajeshi hao.
Wapiganaji wa kiisilamu waliteka eneo la Kaskazini mwa nchi mwaka jana lakini wamekuwa wakishindwa tangu majeshi ya Ufaransa kuanza kuwashambulia mapema mwezi huu.

Mwandishi wa BBC nchini Mali anasema Wafaransa wanatarajiwa kuikomboa Timbuktu bila ya tatizo.

Ndege za Ufaransa piya zimeshambulia mji wa Kidal ambako ndiko wapiganaji walianza uvamizi wao mwezi Machi mwaka jana.
Jumamosi wanajeshi wa Ufaransa na Mali waliukomboa mji wa Gao uliokuwa ngome ya wapiganaji.
Na Mali ndio swala muhimu linalojadiliwa kati ya viongozi wa nchi za Umoja wa Afrika, AU, wanaokutana mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Sasa nchi zaidi za Afrika zinatarajiwa kuchangia wanajeshi katika kikosi cha kimataifa kitachokwenda Mali, mbali ya wale walioshafika nchini humo.