NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Friday, March 29, 2013

USHIRIKINA!


Na Mwandishi Wetu, Mbeya
HII inasikitisha na inashangaza sana!
MWANAMKE mmoja ambaye ni mke wa mtu aliyejulikana kwa jina la Atupele mkazi wa Mtaa wa Masewe Kata ya Ilemi, jijini hapa, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya wakazi wa eo hilo kumpa kibano wakimtuhumu kwa ushirikina.
Mama Atupele anayetuhumiwa kwa ushirikina
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni baada ya mtoto aliyetambuliwa kwa jina la Judith Chengula (3) kupotea katika mazingira ya kutatanisha, Februari 22, mwaka huu.
Kwa mujibu wa wakazi hao, mtoto huyo alipotea majira ya saa 11 jioni wakati alipokuwa akitoka kanisani na dada yake aitwaye Anitha Mgaya.
Imeelezwa kwamba, baada ya wazazi, ndugu, jamaa na marafiki kumtafuta Judith bila mafanikio, walikaa vikao kadhaa lakini Atupele hakuhudhuria.
Habari zinadai kwamba, kitendo cha mtuhumiwa huyo kutohudhuria kwenye vikao hivyo kiliwapa mashaka na kuhisi huenda mama huyo anahusika na kupotea kwa Judith.
Imedaiwa kwamba Machi 23, mwaka huu asubuhi wananchi hao waliendelea kusisitiza Atupele achukuliwe hatua lakini baadaye waliamua kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alidai kuwa, baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwa mama huyo walikuta vitu vilivyodaiwa ni vitovu vya watoto wachanga, hivyo kuamsha hasira kwa raia.
“Mama huyo alipobanwa alijikuta akibabaika ndipo watu wakamvaa kabla ya kuokolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa huo, Nedy Mwamlima aliyempeleka polisi kwa usalama wake.
“Kwa hasira, wananchi wa aneo hilo waliingia ndani ya nyumba ya mama huyo na kutoa nje vitu mbalimbali kisha kuvichoma moto, pia walibomoa nyumba yake na kuharibu mazao yaliyokuwa nje ya nyumba hiyo,” alisema shuhuda huyo.
 Hata hivyo, gazeti hili linalaani watu kujichukulia sheria mkononi na kwamba, yanapotokea mazingira kama hayo ni vyema vyombo vya dola vikataarifiwa ili viweze kuchukua hatua sahihi badala ya kile walichokifanya wananchi wa eneo hilo-Mhariri.

KAMA UMESALITIWA, FANYA HAYA KABLA YA KUMUACHA!


Suala la wapenzi au wanandoa kusalitiana limekuwa likiwaumiza walio wengi na baadhi wanaposalitiwa hujikuta wakichanganyikiwa na wengine kuchukua maamuzi ya kukatisha maisha yao.
Hakuna anayeweza kusema kuwa, haumii anaposalitiwa na kama yupo basi huyo aliyenaye hampendi kwa dhati.
Kama unampenda, akikusaliti lazima utaumia lakini cha kujiuliza ni kwamba, tukishasalitiwa ndiyo mwisho wa maisha yetu? Tukisalitiwa na wapenzi wetu suluhisho ni kunywa sumu?
Sidhani kama hayo ni maamuzi ya busara. Yapo ya kufanya unapokumbwa na balaa hili la kusalitiwa na leo nimeona nikupe dondoo chache zinazoweza kukusaidia.
Kwanza, kubaliana na kilichotokea. Kama ameshakusaliti ni tukio ambalo limeshatendeka na huwezi kufanya chochote kulifuta. Kwa maana hiyo kubali kuwa umetendwa na kwa kuwa una moyo wa kibinadamu, huzunika mwisho liache lipite ili uweze kujipanga upya.
Pili, usijalaumu. Kuna ambao wakishasalitiwa huanza kujilaumu ni kwa nini waliingia kwenye uhusiano na watu waliowatenda. Utamsikia mtu akisema; ‘Najuta kumpenda fulani’. Kujilaumu kwa namna hiyo hakutakiwi kwani kutakufanya uzidi kupata maumivu moyoni mwako na kunyong’onyea.
Tatu, jifanye kama vile aliyesalitiwa siyo wewe bali ni rafiki yako kisha jiulize ungemshaurije? Ushauri ambao ungempatia basi uchukue kisha ufanyie kazi.
Kujitoa kwako kwenye tatizo kunaweza kukupunguzia machungu kwa kiasi fulani licha ya kwamba si kazi rahisi.
Nne, je, kitendo cha mpenzi wako kukusaliti kimekukosesha imani juu yake? Kama ni hivyo, unadhani una sababu ya kuendelea kuwa naye au unahisi madhara aliyokupatia huwezi kumvumilia?
Kama utapata jibu ni vyema ukachukua uamuzi ambao nafsi yako itaona ni sahihi.
Tano,usione hatari kumpasha ukweli. Kwa vyovyote utakavyoamua ni lazima umweleze namna alivyokuumiza kwa usaliti wake. Hata kama utampa nafasi nyingine lazima ajue jinsi alivyokuumiza ili iwe changamoto kwake.
Sita, jaribu kuchunguza ili kujua kwa nini amefikia hatua ya kukusaliti. Usiliache likapita hivihivi, unatakiwa kujua sababu ya yeye kukusaliti. Je, kuna ambacho anakikosa kwako au ni tamaa zake tu? Jibu utakalolipata litakusaidia katika maisha yako ya kimapenzi.
Saba, usikubali akuletee usanii katika hilo. Nasema hivi kwa kuwa, huenda huyo mpenzi wako ni ‘mjanjamjanja’ na anaweza kukulainisha kwa maneno ambayo yanaweza kukufanya ukalichukulia poa tukio hilo. Kuwa na msimamo na eleza hisia zako kwa uwazi.
Nane, ni vyema ukachukua uamuzi sahihi. Kama amekusaliti, uamuzi wa kuendelea kuwa naye au kumuacha uuchukue bila shinikizo. Hata kama kakuumiza, kama unadhani unaweza kumpa nafasi nyingine mpe ili usije ukajuta baadaye kwa kumkosa lakini kama unaona moyo wako unasita, muache.
Tisa, unayo nafasi ya kumsamehe licha ya kwamba utakuwa umeachana naye. Hii itakusaidia kuliondoa dukuduku lako moyoni na kujiepusha na kukosa amani.
Kumi, chukulia tukio hilo kama fundisho kwako. Huenda wewe ndiye uliyechangia kusalitiwa, kama ni hivyo badilika ili yasije yakakukuta kama hayo utakapokuwa na mwingine. Pia kama kusalitiwa kumetokana na kutoridhika kwa mpenzi wako, kuwa makini wakati wa kuchagua mwingine wa kuwa naye.

FLAVIANA MATATA ATUMIKA KUTAPELI MTANDAONI

Stori: Hamida Hassan
Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata amekuwa akitumiwa na watu wasiojulikana kuwatepeli watu kupitia mtandao wa Facebook kwa akaunti yenye jina la Flaviana Matata’s huku ikidaiwa kuwa wengi wameshalizwa.
Taarifa ya Kampuni ya Compass Communications inayosimamia kazi za modo huyo inaeleza kuwa, watu hao wasiojulikana wamefungua akaunti kwenye mtandao wa Facebook na kuwarubuni watu kuwa, ‘Flaviana’ huyo anawatafutia kazi wasichana nje ya nchi kwa gharana ya shilingi hadi 200,000.
“Tunawatahadharisha watu kuwa Flaviana hatafutii wasichana kazi ya uanamitindo, wanaotumia akaunti ya Flaviana Matata’s ni genge la wahalifu, akauti sahihi ya Flaviana ni Flaviana Lavvy Matata,” ilieleza taarifa hiyo.

RECHO: SINA UHAKIKA WA KUOLEWA NA SAGUDA

Stori: Gladness Mallya
MSANII wa filamu Bongo, Rachel Haule ‘Recho’ amefunguka kuwa japokuwa wamekaa kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa muda mrefu na mpenzi wake George Saguda bado hana uhakika kama ndiye atakayemuoa.
Akichonga na paparazi wetu, Recho alisema kuwa kutoka moyoni anampenda Saguda na anatamani siku moja awe mume wake ila kufanikiwa wao kuoana anamuachia Mungu kwani ndiye anayepanga kila jambo
 “Suala la ndoa namuachia Mungu kwa sababu wapo mastaa wengi waliochumbiwa lakini wameishia kuzalishwa na kuachwa hivyo mimi naamini kama Mungu amenipangia Saguda awe mume wangu atanioa lakini kama siyo basi siwezi kulazimisha,” alisema Recho.

Thursday, March 28, 2013

UNAPOPATA FEDHA, ‘USIZITUMBUE’ KANA KWAMBA KESHO HAIPO!


Leo nataka kuzungumzia tabia ya baadhi ya watu kutumia fedha wanazozipata kwa fujo kana kwamba wameambiwa kuwa kesho wanakufa. Hakuna asiyefahamu umuhimu wa pesa, na kutokana na hilo, wengi wamekuwa wakipambana usiku na mchana kuhakikisha wanazipata.
Cha ajabu sasa, wapo ambao wanatumia nguvu na akili zao kuzitafuta fedha hizo lakini mwishowe wanazimwaga kwa matumizi yasiyo na mbele wala nyuma.
Utakubaliana na mimi kwamba wapo watu ambao leo hii wanashinda wakibeba zege, kuzibua mitaro, kubeba mizigo na kazi nyingine nzito lakini jioni wanapopata ujira hukimbilia baa na kuzitumbua kwa staili ya lete kama tulivyo.
Ninachokizungumza kipo huko mtaani, watu wanatumia pesa kama vile wana uhakika wa kuendelea kuzipata kila siku. Ndiyo maana nadiriki kusema kwamba kutumia pesa ovyo ni sawa kabisa na kujiandalia ufukara wa baadaye.
Wapo watu wengi tu ambao kwa sasa ni mafukara wa kutupwa lakini utakapojaribu kuangalia historia yao huko nyuma utagundua walikuwa na pesa nyingi ila walikuwa wakizutumia kana kwamba wanamkomoa mtu lakini leo wanaishi maisha ya kuungaunga, hawana mwelekeo.
 Sikatai kwamba matumizi ya mtu yanatokana na kipato chake na ndiyo maana mtu anayepokea mshahara wa shilingi milioni moja kwa mwezi hawezi kuwa na matumizi sawa na mtu anayepokea laki moja lakini je, kuwa na kipato kikubwa ndiyo kukufanye utumie fedha zako ovyo eti kwa sababu tu una uhakika wa kupata nyingine mwezi ujao?
Jamani tukumbuke kwamba, maisha ni kupanda na kushuka. Leo hii unafanya kazi katika kampuni ama shirika fulani lakini uwezekano wa kuwepo katika shirika hilo kwa kipindi chote cha maisha yako ni mdogo. Unaweza kuachishwa kazi wakati wowote.
Sasa kama ulikuwa unatumia ovyo pesa uliyokuwa unaipata, unatarajia nini kama siyo kuingia kwenye ufukara ambao kwa kiasi fulani ungeweza kupunguza ukali wake kama ungekuwa makini katika matumizi ya pesa zako?
Utumiaji ovyo wa pesa ni kuzitumia bila mpangalio tena wakati mwingine katika mambo ambayo si ya msingi lakini tutambue kwamba, ufujaji wa pesa hauko katika anasa tu kama vile ulevi, kuhonga na mambo mengine kama hayo, bali pia katika mambo ambayo hata yakikosekana hayawezi kuleta athari.
Tafiti mbalimbali zimeonesha kwamba, wengi ambao hutumia pesa ovyo ni athari za malezi waliyoyapata kutoka kwa wazazi wao tangu utotoni. Mzazi ndiye anayeweza kumfundisha mtoto wake kutokuwa na nidhamu katika pesa.

Itaendelea wiki ijayo.

Thursday, March 21, 2013

HAWA NDIYO... ‘WATAALAM’ WA PICHA ZA UTUPU BONGO


Makala na Erick Evarist
NCHI za wenzetu staa kupiga picha za utupu si kitu kigeni lakini Kibongobongo sheria na maadili ya Mtanzania hayaruhusu kufanya hivyo.
Licha ya kubanwa na sheria pamoja na maadili, wapo wasanii ambao kwa nyakati tofauti walijikuta katika adha ya kupigwa kama si kujipiga picha za utupu kisha zikazagaa mitaani.
Wapo waliotajwa kupiga picha hizo kwa kusaka umaarufu, waliopigwa na wapenzi wao kisha wakazivujisha lakini wengine imedaiwa kuwa wamezivujisha wenyewe na kusingizia zimevujishwa na wapenzi wao.
Ifuatayo ni orodha ya wasanii mbalimbali Bongo ambao waliwahi kukwaa skendo ya picha za utupu:
Wema Sepetu:
Mwaka 2010 picha yake ya utupu ilizagaa mtandaoni huku ikidaiwa kuwa chanzo cha kusambaa kwake ni boifrendi wake ambaye alimpiga na kuzisambaza. Kama hiyo haitoshi, mwaka huu mrembo huyo alidaiwa kuposti picha zake nyingine za utupu katika mtandao wa Instagram.
Diana Hussein:
Huyu  ni Miss Dar Indian Ocean ambaye pia ni Miss Kinondoni namba 2 mwaka jana, mrembo huyo hivi karibuni amejikuta akipata aibu baada ya picha yake ya utupu kuvuja. Ilidaiwa kuwa alifanya hivyo kwa azma ya kusaka umaarufu.
Jack wa Chuz:
Ni bonge la ‘actress’ Bongo Movie, mwaka 2012 alipigwa picha za utupu na kusambazwa kila kona ya Jiji la Dar. Ilidaiwa kuwa kuna mtu alizichukua picha hizo kutoka kwenye simu yake na kuzisambaza kwenye vyombo vya habari.
Agness Masogange:
Nini picha! Yeye ilivuja video yake ya utupu kabisa. Ilisambaa kama njugu katika mitandao ya kijamii mwaka jana. Vyanzo makini vilidai kuwa video hiyo alipigwa na mpenzi wake na haikujulikana mara moja chanzo kilichozivujisha.
Jacqueline Wolper:
Pamoja na heshima kubwa aliyonayo kwenye soko la filamu, mapema mwaka huu staa huyo amejikuta akichafuka baada ya picha yake ya utupu kuanikwa gazetini. Ilidaiwa kuwa picha hiyo alipigwa kwenye bethidei ya msanii mwenzake.
Marry John:
Msanii wa filamu Bongo, Mary John ‘Maua’ mwaka jana alijipatia jina baada ya kupiga picha kadhaa za utupu na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii yeye mwenyewe.
Aunt Lulu:
Mara kadhaa amekuwa akitengeneza vichwa vya habari magazetini kwa kupiga picha za utupu. Mfano hai ni picha ambazo alipiga mwaka jana, ambapo alidai kuwa alipigwa bichi alipokwenda ‘kula bata’.
Lulu:
Mwaka 2010 alijikuta akichafuka kwa kutajwa kwenye skendo ya kupiga picha ya utupu. Alipoulizwa kuhusiana na picha hiyo alikanusha kuwa si ya kwake na kudai kuwa ilitengenezwa na watu ili kumchafua.
Jack Patrick:
Kwa upande wake suala la kuvuja kwa picha zake za utupu siyo ishu. Mwaka jana ilidaiwa kuwa aliziposti picha zake za utupu kwenye mtandao wa BBM, haileweki ni kwa nini huwa anafanya hivyo.
Isabela ‘Vai wa Ukweli’:
Huyu ni chipukizi kwenye anga la filamu Bongo, mara kadhaa amepigwa picha za utupu na kusambazwa kwenye vyombo vya habari. Imedaiwa kuwa hufanya hivyo kama kutafuta mlango wa kutokea kwenye ustaa.
Maadili ya Mtanzania yanatukataza kufanya vitendo vya namna hii hivyo ni vyema wahusika wakawa makini, waepuke kupiga wala kuhusika kusambaza picha zao za utupu kwa namna yoyote ile.      

UKATILI 100%

Na Patrick Mabula, Kahama
HUU ni ukatili kwa 100%! Martha Charles (22), mkazi wa Nyahanga wilayani hapa ambaye ni mtumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama ameuawa kinyama kwa kuchinjwa shingoni na mume wake, Amani lina habari ya kusikitisha.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga, Afande Onesmo Lyanga alisema tukio hilo lilitokea katikati ya wiki iliyopita ambapo pia alimtaja mume anayedaiwa kutekeleza unyama huo kuwa ni Asack Nzolela (29), mfanyabiashara wa bucha la nyama ya ng’ombe.
Afande Lyanga alisema mtuhumiwa alimchinja  mkewe wakiwa wamelala chumbani kwenye nyumba ya wazazi wa mwanaume huyo na baada ya kufanya ukatili huo alikimbia.
Habari za uhakika zilizopatikana kutoka katika familia ya marehemu zilisema chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi wa kifamilia ambapo mtuhumiwa alianza kwa kumlaumu mama yake mzazi kwa kitendo cha kumtafutia kazi mkewe katika Halmashauri ya Mji wa Kahama wakati yeye alikuwa hataki mkewe afanye kazi.
Habari zilizopatikana eneo la tukio kutoka kwa mmoja wa ndugu anayeishi na familia hiyo, Paul Edward alisema mbali na kuchinjwa shingoni pia marehemu alikatwakatwa sehemu mbalimbali za mwili wake.
Edward alisema usiku wa tukio akiwa amelala katika moja ya chumba ndani ya nyumba hiyo, alisikia kelele za ugomvi kutoka kwenye chumba cha wanandoa hao hali iliyomfanya apige kelele zilizowafikia majirani ambao walifika kutoa msaada.
Akasema majirani hao sanjari na yeye walimkuta mtuhumiwa ameshamchinja mkewe kwa kisu na kutoweka kusikojulikana.
Nao majirani waliokwenda kutoa msaada ambao hawakupenda majina yao yatajwe gazetini, walisema walikuta mwili wa Martha ukiwa kitandani huku amekatwa na kitu chenye ncha kali katika eneo lote la shingo, ndipo walipomchukua na kumkimbiza hospitali lakini tayari alikuwa ameshakata roho.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, Noel Mkisi alisema baada ya muuaji huyo kutoroka usiku huohuo jitihada za kumsaka zilianza.
Tukio la kuchinjwa kinyama kwa mwanamke huyo limetokea siku chache baada ya hivi karibuni, mchuna ng’ombe Musa Petro (27) naye kumuua kwa kumchinja kwa kisu mpenzi wake, Jessica Elialinga (19).
Naye Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Maduka ya Nyama Kahama, Faraji Mohamed akiongea na gazeti hili alisema Petro ni mfanyakazi wa Nzolela katika duka lake la nyama (bucha) ambapo alishangaa kusikia Nzolela amemchinja mke wake kama alivyofanya mfanyakazi wake, Petro.
Wakati tunakwenda mitamboni habari zilizopatikana kutoka Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Kahama na kudhibitishwa na OCD George Simba zilisema mtuhumiwa huyo amekamatwa.

Friday, March 15, 2013

WAGANGA 12 KUMTIBU JAY DEE

Na Hamida Hassan
WAGANGA wanaodai kuwa ni wataalam na wana uzoefu wa kupambana na jini mahaba linalomsumbua Mwanamuziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, wamejitokeza huku kila mmoja akiomba apewe nafasi ya kumtibu bure.
Mwanamuziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’.
Baada ya gazeti hili toleo lililopita kuingia mtaani na stori inayoeleza jinsi jini mahaba anavyomsumbua Jide, watu wapatao 12 waliojitambulisha kuwa ni wataalam wa mambo hayo waliomba kuunganishwa na mke huyo wa Mtangazaji wa Radio Times FM, Gardner G. Habash huku wakiahidi kumtibu bila gharama yoyote.
Mmoja wa wataalam hao aliyejitambulisha kwa jina la Jumaa wa Magomeni, Dar alisema: “Nimesoma habari kuhusu Jide, mimi naweza kumtibu tena bure, mpe namba yangu na mwambie anipigie.”
Mwingine ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alisema: “Nimesikitika sana kusoma hii habari ya huyu msanii Lady Jaydee, kwa kifupi naweza kumtibia free of charge.”
Kufuatia maombi ya wataalam hao, mwandishi wetu alijitahidi kumtafuta Jide bila mafanikio lakini juzikati kupitia kipindi chake cha Diary ya Lady Jaydee alionekana akipewa matibabu na ustaadhi mmoja, mazingira yanayoashiria kuwa huenda mambo yametulia.

KHADIJA YUSUF AJIFUNGUA, MTOTO AFARIKI TENA!

Na Mwaija Salum
KWA mara nyingine tena, mwimbaji wa Kundi la Jahazi Modern Taarab la jijini Dar, Khadija Yusuf amejifungua na mtoto kufariki dunia, Ijumaa limetonywa.
Khadija Yusuf.
Habari hizi za masikitiko zimepokelewa katika chumba chetu cha habari Jumatano iliyopita na kuthibitishwa na wadau wa mbalimbali wa muziki wa taarab.
“Khadija amejifungua katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili lakini mtoto si riziki,” amesema mmoja wa wadau wa muziki huo.
Mwanzoni mwa mwaka jana, mwimbaji huyo aliyewahi kuimbia makundi ya The East African Melody, Zanzibar Stars na Five Stars alijifungua kwa upasuaji baada ya kusumbuliwa na presha lakini mtoto alifariki dunia.
Hii ni mara ya tatu kwa Khadija kupoteza watoto katika uzazi, mwaka jana alipewa onyo na daktari kwamba asishike mimba mpaka baada ya miaka mitatu lakini hakutii agizo hilo.

Thursday, March 14, 2013

DENTI ALIYEPIGA PICHA ZA UTUPU ADAIWA KUTENGWA NA FAMILIA

Na Mwandishi Wetu
YULE denti wa chuo kimoja jijini Mwanza ambaye wiki iliyopita tuliandika habari ya picha zake za utupu kuzagaa kwenye mtandao wa BBM, Fatuma Omari amejikuta kwenye wakati mgumu kufuatia madai kuwa familia yake imemtenga.
Denti Fatuma Omari akiwa katika pozi.
Chanzo chetu kilichoomba hifadhi ya jina lake kilidai kuwa, mara baada ya kutoka kwa habari hiyo, baadhi ya ndugu zake walikasirika na  kutaka kujua undani wake.
“Ile stori ilipotoka ndugu wa Fatuma hawakuamini kuwa kweli kapiga picha hizo.
“Kwa bahati kuna mtu aliyekuwa na picha hizo, walipoziona, waliumia sana na baadhi wakafikia hatua ya kusema hawana radhi naye,” kilidai chanzo hicho.
Ijumaa lilimtafuta Fatuma ili kuzungumzia madai hayo bila mafanikio ila kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Saleh baada ya stori kutoka, alilipigia simu Ijumaa na kusema:
“Fatu ni mdogo wangu, nashangaa mmemuandika kuwa kapiga picha chafu wakati siyo kweli. Kama hizo picha zipo nitakuja kuziona laa sivyo tutapelekena mahakamani,” alisema Saleh.
Tumeamua kutumia picha hiyo chafu hapo chini aliyopiga Fatuma ili kuonesha uhalisia.

Tuesday, March 12, 2013

HUYU NDIO BIBI MWAFRIKA JASIRI ALIEKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA ALIZOFICHA KICHWANI.


.
.
Giwa Ayoka Sikirat ni bibi mwenye umri wa miaka 53 ambae amekamatwa na kikosi maalum cha kuzuia dawa za kulevya huko Nigeria akiwa amezificha dawa za kulevya kwenye nywele kichwani na kuzifunika.
Alikamatwa kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abuja akiwa anaelekea Pakistan kwa kupitia Addis Ababa na Dubai ambapo pia aliemsindikiza Uwanja wa ndege amekamatwa, ni Joseph mwenye umri wa miaka 59.
Bibi huyo ambae anaonekana jasiri, imefahamika alishawahi kuhudhuria shule ya Fashion na maswala ya nywele huko Lagos mwaka 1994.

HIZI NDIO STORI NZITO ZA MAGAZETI YA LEO MARCH 12 2013, KURASA ZA MWANZO NA MWISHO



.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC02125 DSC02126 DSC02127 DSC02128 DSC02129
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Neno La Leo: Nahofia, CCM Na Wapinzani Hawana Cha Kujifunza Kutoka Kenya!‏


Ndugu zangu,
Uchaguzi Mkuu wa Kenya umefuatiliwa kwa karibu sana na sisi Watanzania, ni pamoja na wanasiasa wa vyama vya siasa; Chama tawala, CCM na wapinzani.
Lakini, nahofia, kuwa hakuna ambacho vyama hivi vyetu vya siasa vitajifunza kutoka Kenya.
Ndio, pamoja na mapungufu ya hapa na pale, lakini Wakenya, kupitia Uchaguzi wao wametuachia somo kubwa sana; kuwa hata Afrika tunaweza kuendesha siasa za kistaarabu ikiwemo chaguzi Huru.
Ni kawaida kwa majirani sisi; Kenya na Tanzania, kuoneana wivu kwenye kupiga hatua kimaendeleo. Hakika ni wivu wa kimaendeleo tunaopaswa kuwa nao. Nikiri, safari hii, kama Mtanzania, nimejisikia kuwaonea wivu Wakenya kwa jinsi walivyoionyesha Afrika na Dunia kuwa nao wanaweza kuwa Taifa Kubwa; kisiasa na kiuchumi.
Mchakato ule wa mabadiliko ya Katiba yao na hata kufanya uchaguzi ule kwa amani na uwazi ni USHINDI mkubwa wa kimfumo. Ni ushindi wa Wakenya wote. Kwamba Wakenya wameujaribu mfumo mpya. Umeonyesha kuwa unafaa.
Kwa mfano, kufuatilia matokeo ya uchaguzi ule kutoka kwenye Tume yao Huru ilikuwa ni kama ‘ burudani’ ya kisiasa. Kila kitu kilikuwa kinawekwa wazi na kisayansi.
Si ajabu Wakenya waliweza kusubiri matokeo kwa juma moja bila kurushiana mawe. Na hata kama ingekuwa kusubiri kwa majuma mawili, naamini kuwa Wakenya wale wangesubiri bila kupigana, maana, wamekuwa na imani kubwa na Tume yao Huru ya Uchaguzi. Na hatukusia kule Kenya, habari ya watu ‘ kulinda kura’ wala kusimama hatua mia moja kutoka kituo cha kuhesabia kwa usiku mzima. Hiyo kazi iliachiwa Tume Huru ya Uchaguzi walioiamini.
Ndio, Wakenya wamejifunza kutokana na ujinga wa wanasiasa wao uliopelekea vurugu za baada ya Uchaguzi wa mwaka 2007. Wengi walikufa na wengine kupoteza makazi na mali zao. Wakaanza haraka mchakato wa kuifanyia marekebisho makubwa Katiba yao. Wakapata Katiba Mpya 2010. Wakenya wale wametumia gharama kubwa kwa kuitafuta amani yao. Kimsingi, tangu 2010, Wakenya wamekuwa ‘ wakiangushiwa mabomu ya ujumbe wa amani’- Ni kila kukicha.
Serikali yao imetumia fedha nyingi sana kufikisha ujumbe wa amani kwa Wakenya. Sasa wanavuna walichopanda; kuwa na chaguzi huru za amani na utulivu. Na walichokitafuta Wakenya kwa gharama kubwa, kwa maana ya amani, sisi Watanzania tulikuwa nayo, sasa tunaipoteza wenyewe ili baadae tuanze kugharamia kuitafuta. Ni ulimbukeni.
Kwa kupitia Katiba yao ya sasa Wakenya wameweza kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ukabila. Kwa namna gani?
Ona kwenye kugombea Urais; mgombea lazima afikishe asilimia 50+1 ( Asilimia 50 na kura moja) ili aweze kutangazwa mshindi. Mgombea pia lazima akubalike kwa asilimia 25 ya Counties zote ( Majimbo yote).
Sasa basi, kwa Kenya, Wakikuyu ni asilimia 23 ya Wakenya. Wajaluo asilimia 11.
Nyingine zilizobaki ni za makabila mengine madogo madogo. Hivyo, ili mgombea ushinde zaidi ya asilimia 50 una lazima ya kukubalika kwenye maeneo mengine nje ya wigo wa kabila lako. Kwamba kula za Wakikuyu pekee kwa Uhuru Kenyatta zisingetosha, vivyo hivyo kwa Odinga.
Utaratibu huo unaua ukabila na kujenga vema misingi ya Utaifa. Hata kama itachukua muda kufika mbali zaidi katika hilo lakini Wakenya wameanza kuondokana na ukabila kwenye siasa zao, kwa kupitia Katiba.
Kwa mantiki hiyo hiyo, Watanzania tungeweza kabisa kuondokana na siasa za udini kwa kuweka, kwenye Katiba yetu ijayo sharti la mgombea Urais kushinda kwa asilimia 50+1 ( Asilimia 50 jumlisha kura 1). Hilo lingewafanya wanasiasa wetu wenye kuwania Urais na vyama vyao pia ‘ Kutia akili’.
Maana ingekuwa na tafsiri moja kuu; kuwa mgombea na chama chenye kuendekeza udini kisingekuwa na nafasi ya kutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wala nafasi ya kushika dola. Maana, hakuna dini hapa Tanzania yenye idadi ya waumini wanaovuka asilimia 50 ya jumla ya Watanzania.
Kwa maana, hiyo, muarobaini wa kumalizana na udini uko kwenye Katiba ijayo, kama tuna nia ya dhati ya kutoka hapa tulipo. Vinginevyo, udini huu tunaosema kuwa ni tatizo tutakuwa tunaulea wenyewe.
Hata tatizo la siasa za ukanda nalo litapotea, maana, hakutakuwa na mgombea au chama kitakachoweza kushinda na kutoa Urais kwa kuegemea kura za kikanda. Hakuna kanda itakayovuka peke yake asilimia 50 ya kura zote. Chama na mgombea kitahitaji kuungwa mkono na wapiga kura wa kanda hata zilizo nje ya anakotoka mgombea Urais.
Vinginevyo, kama alivyotamka Uhuru Kenyatta kwenye hotuba yake nzuri iliyojaa utaifa hivi majuzi, kuwa katika uchaguzi waliofanya, kila kura ilikuwa ina umuhimu. Hivyo, kila kabila lilikuwa na umuhimu. Na Uhuru Kenyatta akaweka wazi anachotaka Serikali yake kwa kushirikiana na Wakenya kufanya ili kuitoa Kenya hapo ilipo na kwenda mbele.
Kenyatata alimalizia na maneno matatu; Forward, Foward. Foward!- Kusonga mbele!
Ndio, Wakenya wameamua; KENYA KWANZA!
And really, The Kenyans are coming, Big Time!
Ni ukweli, Wakenya wanakuja. Kisiasa na kiuchumi. Sisi hatujajipanga na hatutaki kujipanga kwa dhati. CCM na wapinzani, na hata media yetu, kama kawaida, tumerudi kwenye kucheza ‘ Kiduku’ chetu. Hatuna cha kujifunza kutoka Kenya. Tumerudi kwenye mambo yetu ya hovyo hovyo; ni Siasa za Mwembe Yanga na Viwanja Vya Jangwani. Siasa za kupigana vijembe. Siasa za reja-reja- Retail politics.
CCM na wapinzani ni kama vile wapenzi wa soka. Wanaangalia kila siku soka la majuu. Wataongea sana kuhusu soka la majuu lilivyo bora.
Lakini, wakirudi kwenye soka lao, ni yale yale, hawana cha kujifunza na hawataki kujifunza. Ni madudu kwenye kuendesha vilabu na hata kufikia kununua mechi kwa kuhonga marefa, wachezaji na viongozi. Ukisema nini hiki?
Utajibiwa; “Wewe Bongo mpira pesa bwana!” “Mpira fitna!” Ni kama majibu ya wanasiasa, iwe wa CCM au vyama vya upinzani. Nao watakwambia; “Wewe, Bongo siasa pesa bwana!” “ Siasa mizengwe na fitna!”
Naam, nahofia, kuwa CCM na wapinzani hawana cha kujifunza kutoka Kenya!

MUME AMMWAGIA MKEWE PETROLI, AMCHOMA MOTO

Lagos, Nigeria
NINI tafsiri ya uelekeo wa dunia kutokana na matukio ya kutisha? Upo ukatili mkubwa umefanyika nchini Nigeria ambapo mume amemwagia mkewe mafuta ya petroli na kumchoma moto.
Janet Udegba.
Kehinde Adesamuye, 39, mkazi wa Lagos, Nigeria anadaiwa kumchoma kwa moto wa petroli hivi karibuni mkewe Janet Udegba, 35, katika Mtaa wa Ikotun jijini Lagos baada ya kuwa na hasira kutokana na kuhisi kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamume mwingine.
Janet alisema wakati wa tukio hilo, alikuwa katika eneo lake la biashara akiuza vyakula kabla ya Kehinde kufika hapo usiku huo na kumwagia petroli mgongoni kisha kuwasha moto kwa kutumia kibiriti.
Janet na Kehinde.
Hata hivyo, alisema Wanigeria hawatamwachia huru Kehinde kutokana na kile alichokifanya. Akisimulia mgogoro wao, anasema:
“Mume wangu amekuwa na wivu daima. Amekuwa na tabia ya kunipiga kila wakati. Nimejaribu mara nyingi kuachana naye lakini huwa ananitishia kuwa lazima atanidhuru. Niliendelea kuishi naye kwa kuwa nilikuwa na hofu ya maisha yangu, aliwahi kuniambia kuwa sitaweza kutoroka hata siku moja.
Janet.
“Serikali lazima ihakikishe kuwa Kehinde analipa kwa kile alichonifanyia. Mimi ni yatima, ninafanya biashara ya vyakula ili niishi. Sasa nimetumia pesa zangu zote kwa ajili ya matibabu. Kwa kweli kwa sasa nahitaji msaada,” alisema mama huyo huku akitokwa machozi.
Kehinde alijaribu kutuma rafiki zake ili wamwombee msamaha kwa Janet lakini alikataa. Mtuhumiwa huyo anashikiliwa na polisi kwa ajili ya kujibu mashtaka yanayomkabili.