NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Saturday, April 27, 2013

DENTI WA CHUO KIKUU ARUSHA ALIVYOUAWA


Stori:Joseph Ngilisho,Arusha
MWANAFUNZI wa mwaka wa pili  katika Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kilichopo Njiro jijini hapa, Henry Koga, ameuawa kikatili na hivi ndivyo alivyouawa.
Enzi za uhai wa mwanafunzi huyo
Kwa mujibu wa wanachuo wenzake ambao hawakutaka majina yao kuandikwa gazetini, Koga aliuawa kinyama kwa kuchomwa kisu shingoni na kundi la watu wasiofahamika wakati akitoka kujisomea nje ya chuo usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.
Imeelezwa kuwa tukio la kuuawa kwa mwanafunzi huyo lilitokea saa 4 usiku ambapo marehemu huyo akiwa na wenzake walivamiwa na kundi la wahuni wapatao wanne katika eneo la CDA, jirani na chuo hicho na Koga kuchomwa kisu shingoni na kifuani.
Wanachuo wenzake walisema marehemu hakuwa anatoka kwenye starehe kama watu wengine wanavyodai bali alikuwa na wenzake  wakitoka kujisomea nje kidogo ya chuo hicho kwa ajili ya kujiandaa na mitihani na walipofika eneo hilo, wakavamiwa na watu wasiojulikana.
Baada ya tukio hilo, baadhi ya wanafunzi  walijikusanya asubuhi yake na kuanza kuandamana kushinikiza uongozi wa chuo hicho kutoa tamko juu ya vitendo vya uhalifu vinavyojirudia mara kwa mara chuoni hapo.
Kufuatia tukio hilo, wanachuo hao walifanya vurugu kubwa na kumlazimisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo kwenda chuoni hapo, alipofika kulitokea hali ya kutoelewana ambapo walimzomea na kumpiga mawe, hali iliyosababisha polisi kuingilia kati na kuwafyatulia mabomu ya machozi.
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema naye alijitahidi kuwatuliza bila mafanikio huku ikidaiwa yeye ndiyo chanzo cha vurugu hivyo kutakiwa kukamatwa. Mkuu wa mkoa alilazimika kuondoka eneo kuokoa maisha yake.
Naye Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Ibrahimu Kilongo akizungumzia tukio hilo, alisema wanachuo 10 wanashikiliwa na polisi kutokana na vurugu hizo na kwamba uchunguzi unaendelea.

Wednesday, April 3, 2013

PICHA 5 ZA LAANA YA "KANGA MOJA" KATIKA SHOW YA MSANII DIAMOND- BUKOBA


Mambo yanayofanywa na kundi la kanga moja ni ya aibu sana  kwa  sababu  ni  uchafu  unaotendeka  mbele  ya  watoto......

Mwanamke  hujifunga  kanga  moja  tu  bila  chupi  wala  chochote  ndani.Baada  ya  hapo  humwagiwa  maji  kitu ambacho  huanika  kila  kitu  hadharani......

Kama haitoshi, akimwagiwa  maji, wenzie  huanza  kumtia  chupa  matakoni  hali  inayoashiria  VITENDO  VYA  ULAWITI......

Tunawafundisha  nini  watoto???..Tunaifundisha  nini  jamii  na  kizazi  cha  kesho????