NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Monday, May 20, 2013

SIMULIZI YA MACHOZI

Na Gladness Mallya
SAKATA la kijana Bonny Fabian Kavishe kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi baba yake, mzee Livingstone Kavishe akiamini ni mwizi sasa ni simulizi ya machozi kufuatia kusomwa kwa waraka mzito ulioandikwa na mtuhumiwa huyo ambaye bado yupo mahabusu ya Polisi Mlandizi, Bagamoyo, Pwani.
Waraka huo ulizidi kuwatoa machozi baadhi ya waombolezaji siku ya mazishi yaliyofanyika Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, Mkoa wa Kilimanjaro kutokana na maneno yenye huruma ya Bonny kuomba msamaha.
WARAKA ULIANDIKIWA NDANI YA MAHABUSU
Habari zisizo na chenga wala kumulika tochi zinasema, mtuhumiwa akiwa mahabusu aliamua kuandika waraka huo na kumpa ndugu yake mmoja (jina halikupatikana) akimpa maelekezo kwamba usomwe siku ya mazishi ya mzee huyo kabla hajafukiwa kaburini kwa vile yeye hatakuwepo.
“Kwa kweli inauma sana! Jamaa alipoona hatapata ruhusa ya askari ili akashiriki mazishi ya baba yake aliomba karatasi na kalamu na kuandika waraka, akampa ndugu yake mmoja, akamwambia usomwe siku ya mazishi ya marehemu kabla hajafukiwa kaburini,” kilisema chanzo.
MWILI WAAGWA NYUMBANI KWA MTUHUMIWA, WASAFIRISHWA NA WARAKA
Jumatano ya Mei 15, mwaka huu, mwili wa marehemu mzee Kavishe uliagwa nyumbani kwa mtuhumiwa licha ya yeye kutokuwepo na ukasafirishwa kwenda Marangu kwa mazishi.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa kwenye kusafirisha mwili huo ni uwepo wa waraka huo ambao mtuhumiwa aliomba usomwe mbele ya waombolezaji siku ya mazishi.
MANENO NDANI WARAKA NI HAYA
Siku ya mazishi, mwanaume aliyepewa jukumu la kuongea kwa niaba ya familia aliusoma waraka huo huku waombolezaji wakiwa makini kumsikiliza.
Alisema waraka huo umeandikwa kwa mikono ya Bonny Kavishe, licha ya kuzungumzia mambo mengine, aliwaomba msamaha ndugu, jamaa na marafiki kwamba wamsamehe kwa kitendo cha kumuua baba yake.
Alisema alifanya kitendo hicho bila kukusudia na wala hajui nini kiliendelea. Haikuwa nia yake kumtoa uhai baba yake aliyefikia nyumbani kwake Mlandizi kwa ajili ya kusherehekea harusi ya mdogo wa mtuhumiwa huyo iliyofanyika Mei 11, mwaka huu.
WARAKA WAWATOA MACHOZI WAOMBOLEZAJI
Chanzo kinasema: Yaani wakati waraka huo ukisomwa ndugu na jamaa walilia sana ikawa ni machozi mara mbili. Kwanza kwa mzee Kavishe kufariki dunia, pili kwa sababu ya ndugu yao huyo ambaye yuko mahabusu kutokana na kumuua baba yake. Sehemu kubwa ya waraka huo, Bonny alikuwa akiomba msamaha.
MTUHUMIWA AFUNGA KULA NA KUNYWA
Maneno mengine yaliyopatikana ndani ya waraka huo ni mtuhumiwa kusema tangu siku ya tukio hilo, Mei 12, mwaka huu ambapo alikamatwa na kuswekwa mahabusu, hakula wala kunywa kitu chochote kwa muda wa saa 48 kwa sababu akili yake ilikinai kufuata utaratibu wa kibinadamu kufuatia kitendo cha kumtoa uhai baba yake.
TUMEFIKAJE HAPA?
Mzee Kavishe alitoka Marangu mkoani Kilimanjaro na kufika Mlandizi kwa ajili ya harusi ya mtoto wake ambaye ni mdogo wa Bonny, aitwaye Boniface Fabian Kavishe.
Baada ya harusi kumalizika, familia ilirudi nyumbani kwa Bonny kwa ajili ya kupumzika. Marehemu aliandaliwa chumba chake ambapo aliingia kulala huku akiwatakia usiku mwema wanaye.
Usiku wa saa tisa kuelekea Jumapili, mzee Kavishe aliamka, akatoka kwenda chooni. Alipomaliza alirudi ndani lakini kwa vile macho yake yalikuwa hayaoni vizuri alishindwa kutambua chumba alichokuwa amelala hivyo akajikuta akiingia chumba alicholala mwanaye Bonny na mkewe Eva.
Inadaiwa wakati huo Eva alikuwa macho, ila Bonny alikuwa usingizini. Eva alishtuka kusikia kitasa cha mlango kikishikwa na mtu kuingia, akapiga kelele za mwiziii! Mwizii jamani!
Kelele hizo zilimwamsha Bonny ambaye naye bila kujua, alichukua bastola kutoka kwenye makazi yake na kumfyatulia ‘mwizi’ huyo. Risasi ilichomoka kwa kasi na kumwingia mzee huyo kwenye paji la uso ambapo alianguka chini na kukata roho papohapo.
Baada ya tukio hilo Bonny alitoka kitandani na kwenda kuwasha taa kwa lengo la kumtambua ‘mwizi’ huyo. Hamadi! Kumbe ni baba yake ambaye muda mfupi nyuma walikuwa kwenye cherekochereko za harusi wakila na kunywa kwa furaha.
MKUU WA KITUO AMWELEZEA MTUHUMIWA
Paparazi wetu alipata nafasi ya kuzungumza na Mkuu wa Kituo cha Mlandizi, Bagamoyo, Pwani, Afande Shaban Musa ambapo alikiri kutokea kwa tukio hilo, akasema uchunguzi bado unaendelea na mtuhumiwa mpaka juzi Jumapili anashikiliwa na jeshi hilo.
Akaongeza: Hili kweli ni jambo la kuhuzunisha kwani mtuhumiwa si mtu wa shari, mpole sana lakini nilishangaa siku hiyo kumwona anakimbilia hapa kituoni mwenyewe na kusema amemuua baba yake.”
Marehemu Kavishe alizikwa Mei 17, 2013.
Mungu ailaze pema peponi rojho yake. Amina.

Angalieni Madudu haya ya TBC leo Asubui

Ndugu watanzania wote kwa ujumla leo asubui katika mapitio ya magazeti mtangazaji wa tbc radio alikuwa akisoma vichwa vya habari vya magazeti na alisoma baadhi ya heading nyingi na akafika kwenye habari iliyokuwa inamzungumzia mch.msigwa..na akaanza kuisoma mch.msigwa amwaambia........., ikaishia hapo hapo nilipoweka nukta hizo na hakuendelea kumalizia habari hio na akaendelea na habari zingine...na bila shaka ilikuwa ni habari ya msigwa kumwambia kinana aende mahakamani..
ndugu nina uliza ni nini maana ya mwandishi huyu kutiomalizia habari hiyo..?
na hili si linathibitisha kuwa tbc si chombo tena cha habari cha wananchi..nani chombo cha chama na serikali yake..?
hebu nisaidieni zaidi maana yake nini hii

Saturday, April 27, 2013

DENTI WA CHUO KIKUU ARUSHA ALIVYOUAWA


Stori:Joseph Ngilisho,Arusha
MWANAFUNZI wa mwaka wa pili  katika Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kilichopo Njiro jijini hapa, Henry Koga, ameuawa kikatili na hivi ndivyo alivyouawa.
Enzi za uhai wa mwanafunzi huyo
Kwa mujibu wa wanachuo wenzake ambao hawakutaka majina yao kuandikwa gazetini, Koga aliuawa kinyama kwa kuchomwa kisu shingoni na kundi la watu wasiofahamika wakati akitoka kujisomea nje ya chuo usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.
Imeelezwa kuwa tukio la kuuawa kwa mwanafunzi huyo lilitokea saa 4 usiku ambapo marehemu huyo akiwa na wenzake walivamiwa na kundi la wahuni wapatao wanne katika eneo la CDA, jirani na chuo hicho na Koga kuchomwa kisu shingoni na kifuani.
Wanachuo wenzake walisema marehemu hakuwa anatoka kwenye starehe kama watu wengine wanavyodai bali alikuwa na wenzake  wakitoka kujisomea nje kidogo ya chuo hicho kwa ajili ya kujiandaa na mitihani na walipofika eneo hilo, wakavamiwa na watu wasiojulikana.
Baada ya tukio hilo, baadhi ya wanafunzi  walijikusanya asubuhi yake na kuanza kuandamana kushinikiza uongozi wa chuo hicho kutoa tamko juu ya vitendo vya uhalifu vinavyojirudia mara kwa mara chuoni hapo.
Kufuatia tukio hilo, wanachuo hao walifanya vurugu kubwa na kumlazimisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo kwenda chuoni hapo, alipofika kulitokea hali ya kutoelewana ambapo walimzomea na kumpiga mawe, hali iliyosababisha polisi kuingilia kati na kuwafyatulia mabomu ya machozi.
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema naye alijitahidi kuwatuliza bila mafanikio huku ikidaiwa yeye ndiyo chanzo cha vurugu hivyo kutakiwa kukamatwa. Mkuu wa mkoa alilazimika kuondoka eneo kuokoa maisha yake.
Naye Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Ibrahimu Kilongo akizungumzia tukio hilo, alisema wanachuo 10 wanashikiliwa na polisi kutokana na vurugu hizo na kwamba uchunguzi unaendelea.

Wednesday, April 3, 2013

PICHA 5 ZA LAANA YA "KANGA MOJA" KATIKA SHOW YA MSANII DIAMOND- BUKOBA


Mambo yanayofanywa na kundi la kanga moja ni ya aibu sana  kwa  sababu  ni  uchafu  unaotendeka  mbele  ya  watoto......

Mwanamke  hujifunga  kanga  moja  tu  bila  chupi  wala  chochote  ndani.Baada  ya  hapo  humwagiwa  maji  kitu ambacho  huanika  kila  kitu  hadharani......

Kama haitoshi, akimwagiwa  maji, wenzie  huanza  kumtia  chupa  matakoni  hali  inayoashiria  VITENDO  VYA  ULAWITI......

Tunawafundisha  nini  watoto???..Tunaifundisha  nini  jamii  na  kizazi  cha  kesho????





Friday, March 29, 2013

USHIRIKINA!


Na Mwandishi Wetu, Mbeya
HII inasikitisha na inashangaza sana!
MWANAMKE mmoja ambaye ni mke wa mtu aliyejulikana kwa jina la Atupele mkazi wa Mtaa wa Masewe Kata ya Ilemi, jijini hapa, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya wakazi wa eo hilo kumpa kibano wakimtuhumu kwa ushirikina.
Mama Atupele anayetuhumiwa kwa ushirikina
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni baada ya mtoto aliyetambuliwa kwa jina la Judith Chengula (3) kupotea katika mazingira ya kutatanisha, Februari 22, mwaka huu.
Kwa mujibu wa wakazi hao, mtoto huyo alipotea majira ya saa 11 jioni wakati alipokuwa akitoka kanisani na dada yake aitwaye Anitha Mgaya.
Imeelezwa kwamba, baada ya wazazi, ndugu, jamaa na marafiki kumtafuta Judith bila mafanikio, walikaa vikao kadhaa lakini Atupele hakuhudhuria.
Habari zinadai kwamba, kitendo cha mtuhumiwa huyo kutohudhuria kwenye vikao hivyo kiliwapa mashaka na kuhisi huenda mama huyo anahusika na kupotea kwa Judith.
Imedaiwa kwamba Machi 23, mwaka huu asubuhi wananchi hao waliendelea kusisitiza Atupele achukuliwe hatua lakini baadaye waliamua kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alidai kuwa, baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwa mama huyo walikuta vitu vilivyodaiwa ni vitovu vya watoto wachanga, hivyo kuamsha hasira kwa raia.
“Mama huyo alipobanwa alijikuta akibabaika ndipo watu wakamvaa kabla ya kuokolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa huo, Nedy Mwamlima aliyempeleka polisi kwa usalama wake.
“Kwa hasira, wananchi wa aneo hilo waliingia ndani ya nyumba ya mama huyo na kutoa nje vitu mbalimbali kisha kuvichoma moto, pia walibomoa nyumba yake na kuharibu mazao yaliyokuwa nje ya nyumba hiyo,” alisema shuhuda huyo.
 Hata hivyo, gazeti hili linalaani watu kujichukulia sheria mkononi na kwamba, yanapotokea mazingira kama hayo ni vyema vyombo vya dola vikataarifiwa ili viweze kuchukua hatua sahihi badala ya kile walichokifanya wananchi wa eneo hilo-Mhariri.

KAMA UMESALITIWA, FANYA HAYA KABLA YA KUMUACHA!


Suala la wapenzi au wanandoa kusalitiana limekuwa likiwaumiza walio wengi na baadhi wanaposalitiwa hujikuta wakichanganyikiwa na wengine kuchukua maamuzi ya kukatisha maisha yao.
Hakuna anayeweza kusema kuwa, haumii anaposalitiwa na kama yupo basi huyo aliyenaye hampendi kwa dhati.
Kama unampenda, akikusaliti lazima utaumia lakini cha kujiuliza ni kwamba, tukishasalitiwa ndiyo mwisho wa maisha yetu? Tukisalitiwa na wapenzi wetu suluhisho ni kunywa sumu?
Sidhani kama hayo ni maamuzi ya busara. Yapo ya kufanya unapokumbwa na balaa hili la kusalitiwa na leo nimeona nikupe dondoo chache zinazoweza kukusaidia.
Kwanza, kubaliana na kilichotokea. Kama ameshakusaliti ni tukio ambalo limeshatendeka na huwezi kufanya chochote kulifuta. Kwa maana hiyo kubali kuwa umetendwa na kwa kuwa una moyo wa kibinadamu, huzunika mwisho liache lipite ili uweze kujipanga upya.
Pili, usijalaumu. Kuna ambao wakishasalitiwa huanza kujilaumu ni kwa nini waliingia kwenye uhusiano na watu waliowatenda. Utamsikia mtu akisema; ‘Najuta kumpenda fulani’. Kujilaumu kwa namna hiyo hakutakiwi kwani kutakufanya uzidi kupata maumivu moyoni mwako na kunyong’onyea.
Tatu, jifanye kama vile aliyesalitiwa siyo wewe bali ni rafiki yako kisha jiulize ungemshaurije? Ushauri ambao ungempatia basi uchukue kisha ufanyie kazi.
Kujitoa kwako kwenye tatizo kunaweza kukupunguzia machungu kwa kiasi fulani licha ya kwamba si kazi rahisi.
Nne, je, kitendo cha mpenzi wako kukusaliti kimekukosesha imani juu yake? Kama ni hivyo, unadhani una sababu ya kuendelea kuwa naye au unahisi madhara aliyokupatia huwezi kumvumilia?
Kama utapata jibu ni vyema ukachukua uamuzi ambao nafsi yako itaona ni sahihi.
Tano,usione hatari kumpasha ukweli. Kwa vyovyote utakavyoamua ni lazima umweleze namna alivyokuumiza kwa usaliti wake. Hata kama utampa nafasi nyingine lazima ajue jinsi alivyokuumiza ili iwe changamoto kwake.
Sita, jaribu kuchunguza ili kujua kwa nini amefikia hatua ya kukusaliti. Usiliache likapita hivihivi, unatakiwa kujua sababu ya yeye kukusaliti. Je, kuna ambacho anakikosa kwako au ni tamaa zake tu? Jibu utakalolipata litakusaidia katika maisha yako ya kimapenzi.
Saba, usikubali akuletee usanii katika hilo. Nasema hivi kwa kuwa, huenda huyo mpenzi wako ni ‘mjanjamjanja’ na anaweza kukulainisha kwa maneno ambayo yanaweza kukufanya ukalichukulia poa tukio hilo. Kuwa na msimamo na eleza hisia zako kwa uwazi.
Nane, ni vyema ukachukua uamuzi sahihi. Kama amekusaliti, uamuzi wa kuendelea kuwa naye au kumuacha uuchukue bila shinikizo. Hata kama kakuumiza, kama unadhani unaweza kumpa nafasi nyingine mpe ili usije ukajuta baadaye kwa kumkosa lakini kama unaona moyo wako unasita, muache.
Tisa, unayo nafasi ya kumsamehe licha ya kwamba utakuwa umeachana naye. Hii itakusaidia kuliondoa dukuduku lako moyoni na kujiepusha na kukosa amani.
Kumi, chukulia tukio hilo kama fundisho kwako. Huenda wewe ndiye uliyechangia kusalitiwa, kama ni hivyo badilika ili yasije yakakukuta kama hayo utakapokuwa na mwingine. Pia kama kusalitiwa kumetokana na kutoridhika kwa mpenzi wako, kuwa makini wakati wa kuchagua mwingine wa kuwa naye.

FLAVIANA MATATA ATUMIKA KUTAPELI MTANDAONI

Stori: Hamida Hassan
Mwanamitindo wa kimataifa, Flaviana Matata amekuwa akitumiwa na watu wasiojulikana kuwatepeli watu kupitia mtandao wa Facebook kwa akaunti yenye jina la Flaviana Matata’s huku ikidaiwa kuwa wengi wameshalizwa.
Taarifa ya Kampuni ya Compass Communications inayosimamia kazi za modo huyo inaeleza kuwa, watu hao wasiojulikana wamefungua akaunti kwenye mtandao wa Facebook na kuwarubuni watu kuwa, ‘Flaviana’ huyo anawatafutia kazi wasichana nje ya nchi kwa gharana ya shilingi hadi 200,000.
“Tunawatahadharisha watu kuwa Flaviana hatafutii wasichana kazi ya uanamitindo, wanaotumia akaunti ya Flaviana Matata’s ni genge la wahalifu, akauti sahihi ya Flaviana ni Flaviana Lavvy Matata,” ilieleza taarifa hiyo.