NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Monday, June 17, 2013

BOMU ARUSHA... NJAMA NZITO

Na Joseph Ngilisho, Arusha
NYUMA ya matukio ya kigaidi ambayo yamefululiza kutokea jijini Arusha kuna njama nzito baada ya kuibuka maswali mengi yanayosababisha mahali hapa kutokuwa shwari na salama kufuatia bomu lililolipuliwa Jumamosi iliyopita, Uwazi lina uchambuzi.
Bomu hilo lililipuliwa katika mkutano wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani Kata ya Kaloleni jijini hapa na kusababisha kuvunjika ghafla huku likiua watu wawili na wengine zaidi ya sitini kujeruhiwa.
Mlipuaji alilipua bomu hilo saa 11:50: jioni, dakika chache kabla ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe (pichani) kumaliza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Soweto jijini hapa na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi kisha kuacha maswali mengi.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo aliwataja waliofariki kuwa ni Judith William Mushi (46) ambaye alikuwa Katibu Kata wa Chadema, Kata ya Sokoni One na mkazi wa eneo hilo aliyemtaja kwa jina moja la Justine (16), mkazi wa Sombetini ambaye alifariki katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Tukio hilo ni la pili la bomu kulipuliwa katika mkusanyiko wa watu kwani Mei 5, mwaka huu bomu lililipuliwa katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti jijini hapa na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.

JE, LILIMLENGA MBOWE?
Baadhi ya wanachama wa Chadema waliozungumza na Uwazi walidai kuwa bomu hilo la kurusha kwa mkono lililenga kumuua Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kutokana na sababu za kisiasa.
Wachunguzi walijiuliza kama mlipuaji alikuwa na nia ya  kumuua Mbowe na Lema kwa nini alitupa bomu kwa wananchi wakati viongozi hao walikuwa wanaonekana wakikusanya michango ya fedha kuchangia ununuzi wa maji kwa wasimamizi wao wa uchaguzi ulioahirishwa?
Pia swali lingine, kama hivyo ndivyo, kwa nini mlipuaji alirusha bomu wakati ambao Mbowe na Lema walikuwa wameshuka jukwaani?

CHADEMA WALIJIPIGA BOMU WENYEWE?
Wapo waliodai kuwa hujuma hizo ni mbinu za kisiasa zinazofanywa na wanasiasa wenye ufinyu wa mawazo huku wakijiuliza Chadema wanahusika?
Swali hilo lilijibiwa na baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wakidai kuwa hawawezi kuhusika kutokana na ukweli kwamba hata kiongozi wao, Judith ameuawa na bomu hilo.

MRUSHA BOMU ALIOKOKAJE?
Watu mbalimbali wanajiuliza kama mrusha bomu alikuwa karibu na umati, aliwezaje kufanya unyama huo bila kukamatwa na wananchi waliomuona akirusha?
Pia katika mkutano huo kulikuwa na ulinzi wa polisi waliokuwa wakilinda usalama wa raia, ilikuwaje mrusha bomu huyo ambaye hakukamatwa, akaweza kuwatoroka hata wao (polisi)?

MLIPUAJI BOMU ANATAKA SERIKALI ICHUKIWE?
Wapo waliodai kuwa kama mrusha bomu yupo nje ya siasa, basi zinazofanyika ni njama nzito za kuwagombanisha wananchi na serikali yao ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kitu ambacho serikali inapaswa kufanyia kazi.
“Kuna uwezekano labda ni haya makundi ya kigaidi na waasi kama M-23 na Al-Shaabab yanayolenga kuzivuruga serikali za Afrika Mashariki kwa kuzichonganisha na wananchi wake,” alisema Mzee Minja, kada wa Chadema mjini hapa.
Baadhi ya wananchi walisema mlipuaji alilenga kuua watu wengi na matokeo yake ni kwamba licha ya watu hao wawili kufariki dunia, majeruhi waliolazwa katika hospitali mbalimbali jijini hapa na KCMC mkoani Kilimanjaro, idadi iliyothibitishwa na polisi imefikia 60.
Habari zilieleza kuwa majeruhi wanne, hali zao zilikuwa mbaya huku mtoto, Farad Jamal (7), akiwa katika hali mbaya zaidi kwenye chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika Hospitali ya KCMC.
Mbowe amesema “ tukio hili ni kubwa na lina mambo mengi, chama kitawahudumia majeruhi wote.”
Kufuatia tukio hilo, msimamizi wa uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne, Jimbo la Arusha, Sipora Liana ambaye ni mkurugenzi wa jiji, alitangaza kuahirisha uchaguzi huo uliokuwa ufanyike juzi (Jumapili) hadi Juni 30, mwaka huu.
Liana alisema kuwa kuahirishwa kwa uchaguzi huo ni kutokana na hali tete iliyojitokeza Jumamosi na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kwa mtazamo huo usingeweza kufanyika kutokana na hali ya usalama kuwa mdogo.
Mkuu wa Mkoa, Mulongo alisema kuwa watu kadhaa wanashikiliwa na polisi wakihusishwa na tukio hilo na aliwasihi wananchi waendelee na shughuli zao wakati vyombo vya dola vikiendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

MAJERUHI WAZUNGUMZA
Akisimulia tukio hilo, mmoja wa majeruhi aliyelazwa katika Hospitali ya Seliani, Abdalah Alila (39) alisema kuwa akiwa katika mkutano huo majira ya saa 11.50 jioni, aliona kitu cheusi kikidondoka karibu yake na baadaye alisikia kishindo kizito.
“Ghafla nilijikuta chini na damu zikinichuruzika huku nikishindwa kutembea, nikatambaa kuomba msaada kwa watu waliokuwa wakikimbia hovyo,” alisema.

MRUSHA BOMU
Taarifa zilidai kuwa kuna mtu alionekana akirusha kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu kwenye eneo la jukwaa karibu na gari la matangazo la chama hicho, lakini alipokuwa akifuatiliwa baada ya kutokea mlipuko huo, polisi nao walikuwa wameanza kudhibiti watu kwa kulipua mabomu ya kutoa machozi na kupiga risasi za moto, hali iliyozidisha vurugu.
Hali hiyo ilifanya barabara zote za Jiji la Arusha kujaa watu waliokuwa wakikimbia hovyo.
Kitendo cha watu kukimbia hovyo kuliwafanya polisi wengi kuingia mitaani kudhibiti watu na hivyo nao kulazimika kutumia mabomu ya machozi, hali ambayo ilizidisha taharuki.

BADO HOFU IMETANDA
Pamoja na viongozi kujitahidi kutuliza wananchi lakini bado hali ni tete jijini hapa kwa kuwa watu wana hofu hasa maeneo ambayo yana mkusanyiko wa watu wengi huku wengine wakijitahidi muda mwingi kuwa majumbani mwao.
Wananchi waliozungumza na Uwazi kwa nyakati tofauti kuhusu tukio hilo, wamemuomba Rais Kikwete kufuatilia kwa kina matukio hayo ili maswali yote yanayoulizwa hivi sasa yaweze kujibiwa japokuwa tayari amesema  serikali itafanya kila liwezekanalo kuwasaka waliohusika na kitendo hicho ili washitakiwe.

Tuesday, May 21, 2013

WEZI WA WAUME ZA WATU CHUKUA HIYO!!!


Mwanake mmoja nchini Zimbabwe amekumbwa na balaa la mwaka baada ya kupoteza VIUNGO VYAKE VYA SIRI ( Uke)....
Mwanamke huyo alikumbwa na balaa hilo usiku wa kuamkia tarehe 29 mwezi wa nne mwaka huu...
Kwa mujibu wa mtandao wa Standardmedia, mwanamke huyo alimka usiku na kuelekea chooni kukojoa.Akiwa chooni, alishangaa kuona mkojo hautoki.Alipojichungulia,Ikulu ilikuwa IMEZIBWA..!!!
Taarifa zinadai kwamba, mwanamke huyo alizimia pale pale. 
Kwa mujibu pia wa mtandao wa Zimbabwean ambao nao umeripoti kuhusu tukio hilo, mwanamke huyo anadaiwa kuwa na tabia chafu ya kutembea na waume za watu, hali ambayo ilikuwa ikiwakera wanawake wenzie...
Mtandao huo umedai kwamba , katika siku za hivi karibuni, mwanamke ajulikanaye kwa jina la Mai alimpa ONYO kali mgoni huyo baada ya kugundua kuwa anatoka kimapenzi na mume wake na kumtaka aache mara moja...
Baada ya siku chache kupita tangu onyo hilo litolewe, mwanamke huyo alijikuta amenyofolewa nyeti zake....

Monday, May 20, 2013

Najua Nilikukosea Sana ila Naomba Umuache Huyo Mwanamke, Amin Nitamlea Mtoto Wako Kama wa Kwangu


Hivi wanawake ni watu wa aina gani? naombeni ushauri jamani, nilikuwa na mpenzi akanisaliti akaenda kuolewa na lijibaba nikatafuta mwingine,nimezaa nae mtoto mmoja natunaishi kwa furaha.cha ajabu ameanza kunitumia mesege,mojawapo imeandikwa hivi nanukuu "Najua nilikukosea samahani sana ila naomba umuache huyo mwanamke, amin nitamlea mtoto wako kama wakwangu kumbuka unafahamika mbaka nyumbani familia yangu inanicheka kwa nilichokifanya".huyu mwanamke ninaeshi nae kaona hiyo massage kaniambia nimsamehee na yuko radhi kuondoka....Sasa nifanyaje nishaurini.

SIMULIZI YA MACHOZI

Na Gladness Mallya
SAKATA la kijana Bonny Fabian Kavishe kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi baba yake, mzee Livingstone Kavishe akiamini ni mwizi sasa ni simulizi ya machozi kufuatia kusomwa kwa waraka mzito ulioandikwa na mtuhumiwa huyo ambaye bado yupo mahabusu ya Polisi Mlandizi, Bagamoyo, Pwani.
Waraka huo ulizidi kuwatoa machozi baadhi ya waombolezaji siku ya mazishi yaliyofanyika Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, Mkoa wa Kilimanjaro kutokana na maneno yenye huruma ya Bonny kuomba msamaha.
WARAKA ULIANDIKIWA NDANI YA MAHABUSU
Habari zisizo na chenga wala kumulika tochi zinasema, mtuhumiwa akiwa mahabusu aliamua kuandika waraka huo na kumpa ndugu yake mmoja (jina halikupatikana) akimpa maelekezo kwamba usomwe siku ya mazishi ya mzee huyo kabla hajafukiwa kaburini kwa vile yeye hatakuwepo.
“Kwa kweli inauma sana! Jamaa alipoona hatapata ruhusa ya askari ili akashiriki mazishi ya baba yake aliomba karatasi na kalamu na kuandika waraka, akampa ndugu yake mmoja, akamwambia usomwe siku ya mazishi ya marehemu kabla hajafukiwa kaburini,” kilisema chanzo.
MWILI WAAGWA NYUMBANI KWA MTUHUMIWA, WASAFIRISHWA NA WARAKA
Jumatano ya Mei 15, mwaka huu, mwili wa marehemu mzee Kavishe uliagwa nyumbani kwa mtuhumiwa licha ya yeye kutokuwepo na ukasafirishwa kwenda Marangu kwa mazishi.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa kwenye kusafirisha mwili huo ni uwepo wa waraka huo ambao mtuhumiwa aliomba usomwe mbele ya waombolezaji siku ya mazishi.
MANENO NDANI WARAKA NI HAYA
Siku ya mazishi, mwanaume aliyepewa jukumu la kuongea kwa niaba ya familia aliusoma waraka huo huku waombolezaji wakiwa makini kumsikiliza.
Alisema waraka huo umeandikwa kwa mikono ya Bonny Kavishe, licha ya kuzungumzia mambo mengine, aliwaomba msamaha ndugu, jamaa na marafiki kwamba wamsamehe kwa kitendo cha kumuua baba yake.
Alisema alifanya kitendo hicho bila kukusudia na wala hajui nini kiliendelea. Haikuwa nia yake kumtoa uhai baba yake aliyefikia nyumbani kwake Mlandizi kwa ajili ya kusherehekea harusi ya mdogo wa mtuhumiwa huyo iliyofanyika Mei 11, mwaka huu.
WARAKA WAWATOA MACHOZI WAOMBOLEZAJI
Chanzo kinasema: Yaani wakati waraka huo ukisomwa ndugu na jamaa walilia sana ikawa ni machozi mara mbili. Kwanza kwa mzee Kavishe kufariki dunia, pili kwa sababu ya ndugu yao huyo ambaye yuko mahabusu kutokana na kumuua baba yake. Sehemu kubwa ya waraka huo, Bonny alikuwa akiomba msamaha.
MTUHUMIWA AFUNGA KULA NA KUNYWA
Maneno mengine yaliyopatikana ndani ya waraka huo ni mtuhumiwa kusema tangu siku ya tukio hilo, Mei 12, mwaka huu ambapo alikamatwa na kuswekwa mahabusu, hakula wala kunywa kitu chochote kwa muda wa saa 48 kwa sababu akili yake ilikinai kufuata utaratibu wa kibinadamu kufuatia kitendo cha kumtoa uhai baba yake.
TUMEFIKAJE HAPA?
Mzee Kavishe alitoka Marangu mkoani Kilimanjaro na kufika Mlandizi kwa ajili ya harusi ya mtoto wake ambaye ni mdogo wa Bonny, aitwaye Boniface Fabian Kavishe.
Baada ya harusi kumalizika, familia ilirudi nyumbani kwa Bonny kwa ajili ya kupumzika. Marehemu aliandaliwa chumba chake ambapo aliingia kulala huku akiwatakia usiku mwema wanaye.
Usiku wa saa tisa kuelekea Jumapili, mzee Kavishe aliamka, akatoka kwenda chooni. Alipomaliza alirudi ndani lakini kwa vile macho yake yalikuwa hayaoni vizuri alishindwa kutambua chumba alichokuwa amelala hivyo akajikuta akiingia chumba alicholala mwanaye Bonny na mkewe Eva.
Inadaiwa wakati huo Eva alikuwa macho, ila Bonny alikuwa usingizini. Eva alishtuka kusikia kitasa cha mlango kikishikwa na mtu kuingia, akapiga kelele za mwiziii! Mwizii jamani!
Kelele hizo zilimwamsha Bonny ambaye naye bila kujua, alichukua bastola kutoka kwenye makazi yake na kumfyatulia ‘mwizi’ huyo. Risasi ilichomoka kwa kasi na kumwingia mzee huyo kwenye paji la uso ambapo alianguka chini na kukata roho papohapo.
Baada ya tukio hilo Bonny alitoka kitandani na kwenda kuwasha taa kwa lengo la kumtambua ‘mwizi’ huyo. Hamadi! Kumbe ni baba yake ambaye muda mfupi nyuma walikuwa kwenye cherekochereko za harusi wakila na kunywa kwa furaha.
MKUU WA KITUO AMWELEZEA MTUHUMIWA
Paparazi wetu alipata nafasi ya kuzungumza na Mkuu wa Kituo cha Mlandizi, Bagamoyo, Pwani, Afande Shaban Musa ambapo alikiri kutokea kwa tukio hilo, akasema uchunguzi bado unaendelea na mtuhumiwa mpaka juzi Jumapili anashikiliwa na jeshi hilo.
Akaongeza: Hili kweli ni jambo la kuhuzunisha kwani mtuhumiwa si mtu wa shari, mpole sana lakini nilishangaa siku hiyo kumwona anakimbilia hapa kituoni mwenyewe na kusema amemuua baba yake.”
Marehemu Kavishe alizikwa Mei 17, 2013.
Mungu ailaze pema peponi rojho yake. Amina.

Angalieni Madudu haya ya TBC leo Asubui

Ndugu watanzania wote kwa ujumla leo asubui katika mapitio ya magazeti mtangazaji wa tbc radio alikuwa akisoma vichwa vya habari vya magazeti na alisoma baadhi ya heading nyingi na akafika kwenye habari iliyokuwa inamzungumzia mch.msigwa..na akaanza kuisoma mch.msigwa amwaambia........., ikaishia hapo hapo nilipoweka nukta hizo na hakuendelea kumalizia habari hio na akaendelea na habari zingine...na bila shaka ilikuwa ni habari ya msigwa kumwambia kinana aende mahakamani..
ndugu nina uliza ni nini maana ya mwandishi huyu kutiomalizia habari hiyo..?
na hili si linathibitisha kuwa tbc si chombo tena cha habari cha wananchi..nani chombo cha chama na serikali yake..?
hebu nisaidieni zaidi maana yake nini hii

Saturday, April 27, 2013

DENTI WA CHUO KIKUU ARUSHA ALIVYOUAWA


Stori:Joseph Ngilisho,Arusha
MWANAFUNZI wa mwaka wa pili  katika Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kilichopo Njiro jijini hapa, Henry Koga, ameuawa kikatili na hivi ndivyo alivyouawa.
Enzi za uhai wa mwanafunzi huyo
Kwa mujibu wa wanachuo wenzake ambao hawakutaka majina yao kuandikwa gazetini, Koga aliuawa kinyama kwa kuchomwa kisu shingoni na kundi la watu wasiofahamika wakati akitoka kujisomea nje ya chuo usiku wa kuamkia Jumatano iliyopita.
Imeelezwa kuwa tukio la kuuawa kwa mwanafunzi huyo lilitokea saa 4 usiku ambapo marehemu huyo akiwa na wenzake walivamiwa na kundi la wahuni wapatao wanne katika eneo la CDA, jirani na chuo hicho na Koga kuchomwa kisu shingoni na kifuani.
Wanachuo wenzake walisema marehemu hakuwa anatoka kwenye starehe kama watu wengine wanavyodai bali alikuwa na wenzake  wakitoka kujisomea nje kidogo ya chuo hicho kwa ajili ya kujiandaa na mitihani na walipofika eneo hilo, wakavamiwa na watu wasiojulikana.
Baada ya tukio hilo, baadhi ya wanafunzi  walijikusanya asubuhi yake na kuanza kuandamana kushinikiza uongozi wa chuo hicho kutoa tamko juu ya vitendo vya uhalifu vinavyojirudia mara kwa mara chuoni hapo.
Kufuatia tukio hilo, wanachuo hao walifanya vurugu kubwa na kumlazimisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo kwenda chuoni hapo, alipofika kulitokea hali ya kutoelewana ambapo walimzomea na kumpiga mawe, hali iliyosababisha polisi kuingilia kati na kuwafyatulia mabomu ya machozi.
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema naye alijitahidi kuwatuliza bila mafanikio huku ikidaiwa yeye ndiyo chanzo cha vurugu hivyo kutakiwa kukamatwa. Mkuu wa mkoa alilazimika kuondoka eneo kuokoa maisha yake.
Naye Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Ibrahimu Kilongo akizungumzia tukio hilo, alisema wanachuo 10 wanashikiliwa na polisi kutokana na vurugu hizo na kwamba uchunguzi unaendelea.

Wednesday, April 3, 2013

PICHA 5 ZA LAANA YA "KANGA MOJA" KATIKA SHOW YA MSANII DIAMOND- BUKOBA


Mambo yanayofanywa na kundi la kanga moja ni ya aibu sana  kwa  sababu  ni  uchafu  unaotendeka  mbele  ya  watoto......

Mwanamke  hujifunga  kanga  moja  tu  bila  chupi  wala  chochote  ndani.Baada  ya  hapo  humwagiwa  maji  kitu ambacho  huanika  kila  kitu  hadharani......

Kama haitoshi, akimwagiwa  maji, wenzie  huanza  kumtia  chupa  matakoni  hali  inayoashiria  VITENDO  VYA  ULAWITI......

Tunawafundisha  nini  watoto???..Tunaifundisha  nini  jamii  na  kizazi  cha  kesho????