NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Tuesday, June 18, 2013

Breaking News:Mapambano makali Arusha,Lema amenusurika kufa

Watu waliolipuliwa na bomu katika mkutano wa Chadema jijini Arusha hivi karibuni wakiwa wamelala chini               Arusha Tanzania
HALI tete katika jijini la Arusha muda huu,Polisi wanapiga mabomu ovyo,watu waliokuwa wamekusanyika katika Uwanja wa Soweto wakisubiri kuaga miili ya watu waliofariki dunia katika shambulio la kigaidi wametawanywa kwa mabomu.
Mbali na watu kutawanywa kwa mabomu hayo,Mbunge wa Arusha Mjini Godless Lema menusurika kufa huku gari lake likiharibiwa vibaya mabomu ya Polisi .
Mwandishi wa Habarimpya.com akiwa eneo la tukio ameshuhudia majeruhi kibao wakikimbizwa katika Hospitali ya Mount Meru jijini Arusha.
Barabara kuu ya kuingia mjini imefungwa, mabomu yanapigwa kila kona jijini Arusha Risasi za moto zinatumika.
Akizungumza na Habaimpya.com katika eneo la tukio mmoja wa wahanga wa tukio hilo, Agnes Mosha anasema kwamba hajui walipo ndugu zake wawili waliokuwa katika viwanja hivyo kwa ajili ya kuaga miili ya rafiki zao.
"Dada nisaidie nivuke barabara nikimbie Mount Meru nasikia kuna dada yangu amepigwa bomu na hali yake ni mbaya sana,siwezi kuvuka dada sina nguvu tena jamani"alilalamika Agnes mbele ya Mwandishi wa Habarimpya.com kisha akapoteza fahamu na kuanguka chini.
Hata hivyo baada ya Agnes kuanguka chini hakuweza kuinuka huku watu wakikimbia na kumkanyaga,kulingana na hali kuwa mbaya eneo hilo mwandishi wa Habarimpya.com pia alilazimika kukimbia nakutafuta eneo la kujificha.

No comments:

Post a Comment