Na Hamida Hassan
WAGANGA
wanaodai kuwa ni wataalam na wana uzoefu wa kupambana na jini mahaba
linalomsumbua Mwanamuziki Judith Wambura ‘Lady Jaydee’, wamejitokeza
huku kila mmoja akiomba apewe nafasi ya kumtibu bure.
Baada ya gazeti hili toleo lililopita kuingia mtaani na stori
inayoeleza jinsi jini mahaba anavyomsumbua Jide, watu wapatao 12
waliojitambulisha kuwa ni wataalam wa mambo hayo waliomba kuunganishwa
na mke huyo wa Mtangazaji wa Radio Times FM, Gardner G. Habash huku
wakiahidi kumtibu bila gharama yoyote.
Mmoja wa wataalam hao
aliyejitambulisha kwa jina la Jumaa wa Magomeni, Dar alisema: “Nimesoma
habari kuhusu Jide, mimi naweza kumtibu tena bure, mpe namba yangu na
mwambie anipigie.”
Mwingine ambaye hakupenda jina lake liandikwe
gazetini alisema: “Nimesikitika sana kusoma hii habari ya huyu msanii
Lady Jaydee, kwa kifupi naweza kumtibia free of charge.”
Kufuatia
maombi ya wataalam hao, mwandishi wetu alijitahidi kumtafuta Jide bila
mafanikio lakini juzikati kupitia kipindi chake cha Diary ya Lady Jaydee
alionekana akipewa matibabu na ustaadhi mmoja, mazingira yanayoashiria
kuwa huenda mambo yametulia.
No comments:
Post a Comment