Na Mwaija Salum
KWA
mara nyingine tena, mwimbaji wa Kundi la Jahazi Modern Taarab la jijini
Dar, Khadija Yusuf amejifungua na mtoto kufariki dunia, Ijumaa
limetonywa.
Habari hizi za masikitiko zimepokelewa katika chumba chetu cha habari
Jumatano iliyopita na kuthibitishwa na wadau wa mbalimbali wa muziki wa
taarab.
“Khadija amejifungua katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili lakini mtoto si riziki,” amesema mmoja wa wadau wa muziki huo.
Mwanzoni
mwa mwaka jana, mwimbaji huyo aliyewahi kuimbia makundi ya The East
African Melody, Zanzibar Stars na Five Stars alijifungua kwa upasuaji
baada ya kusumbuliwa na presha lakini mtoto alifariki dunia.
Hii ni
mara ya tatu kwa Khadija kupoteza watoto katika uzazi, mwaka jana
alipewa onyo na daktari kwamba asishike mimba mpaka baada ya miaka
mitatu lakini hakutii agizo hilo.
No comments:
Post a Comment