NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Friday, March 15, 2013

KHADIJA YUSUF AJIFUNGUA, MTOTO AFARIKI TENA!

Na Mwaija Salum
KWA mara nyingine tena, mwimbaji wa Kundi la Jahazi Modern Taarab la jijini Dar, Khadija Yusuf amejifungua na mtoto kufariki dunia, Ijumaa limetonywa.
Khadija Yusuf.
Habari hizi za masikitiko zimepokelewa katika chumba chetu cha habari Jumatano iliyopita na kuthibitishwa na wadau wa mbalimbali wa muziki wa taarab.
“Khadija amejifungua katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili lakini mtoto si riziki,” amesema mmoja wa wadau wa muziki huo.
Mwanzoni mwa mwaka jana, mwimbaji huyo aliyewahi kuimbia makundi ya The East African Melody, Zanzibar Stars na Five Stars alijifungua kwa upasuaji baada ya kusumbuliwa na presha lakini mtoto alifariki dunia.
Hii ni mara ya tatu kwa Khadija kupoteza watoto katika uzazi, mwaka jana alipewa onyo na daktari kwamba asishike mimba mpaka baada ya miaka mitatu lakini hakutii agizo hilo.

No comments:

Post a Comment