Stori: Gladness Mallya
MSANII
wa filamu Bongo, Rachel Haule ‘Recho’ amefunguka kuwa japokuwa wamekaa
kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa muda mrefu na mpenzi wake George Saguda
bado hana uhakika kama ndiye atakayemuoa.
Akichonga
na paparazi wetu, Recho alisema kuwa kutoka moyoni anampenda Saguda na
anatamani siku moja awe mume wake ila kufanikiwa wao kuoana anamuachia
Mungu kwani ndiye anayepanga kila jambo
“Suala la ndoa namuachia
Mungu kwa sababu wapo mastaa wengi waliochumbiwa lakini wameishia
kuzalishwa na kuachwa hivyo mimi naamini kama Mungu amenipangia Saguda
awe mume wangu atanioa lakini kama siyo basi siwezi kulazimisha,”
alisema Recho.
No comments:
Post a Comment