
HII inasikitisha na inashangaza sana!
MWANAMKE mmoja ambaye ni mke wa mtu aliyejulikana kwa jina la Atupele mkazi wa Mtaa wa Masewe Kata ya Ilemi, jijini hapa, amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya wakazi wa eo hilo kumpa kibano wakimtuhumu kwa ushirikina.
Tukio hilo la aina yake lilitokea hivi karibuni baada ya mtoto aliyetambuliwa kwa jina la Judith Chengula (3) kupotea katika mazingira ya kutatanisha, Februari 22, mwaka huu.


Habari zinadai kwamba, kitendo cha mtuhumiwa huyo kutohudhuria kwenye vikao hivyo kiliwapa mashaka na kuhisi huenda mama huyo anahusika na kupotea kwa Judith.


“Mama huyo alipobanwa alijikuta akibabaika ndipo watu wakamvaa kabla ya kuokolewa na Kaimu Mwenyekiti wa Mtaa huo, Nedy Mwamlima aliyempeleka polisi kwa usalama wake.
“Kwa hasira, wananchi wa aneo hilo waliingia ndani ya nyumba ya mama huyo na kutoa nje vitu mbalimbali kisha kuvichoma moto, pia walibomoa nyumba yake na kuharibu mazao yaliyokuwa nje ya nyumba hiyo,” alisema shuhuda huyo.
Hata hivyo, gazeti hili linalaani watu kujichukulia sheria mkononi na kwamba, yanapotokea mazingira kama hayo ni vyema vyombo vya dola vikataarifiwa ili viweze kuchukua hatua sahihi badala ya kile walichokifanya wananchi wa eneo hilo-Mhariri.
No comments:
Post a Comment