Bibi Somoe Issa kushoto, akiwa na mwandishi wa habari wa info radio mjini Mtwara.
Bibi
Somoe Issa (90) mkazi wa kijiji cha Msimbati (pichani kulia) jana
usiku alileta kizazaa baada ya watu wasiojulikana kuchoma gari
lililokusudia kumtorosha bibi huyo baada ya kutoa kauli kuhusu sakata la
gesi , bibi Somoe inasemekana alisema kuwa gesi ikisafirishwa kutoka
Mtwara kwenda Dar es salaam kama serikali ilivyokusudia basi itageuka
kuwa Maji na si gesi tena! Inasemekana bibi huyo alitaka kwenda kuonana
na wazee
wa kimila na kuongea na kuhusu suala zima la gesi, pia imefahamika
kuwepo kwa ulinzi mkali kwenye nyumba ya bibi huyo toka jana mara baada
ya tukio hilo kutokea
Kuwa karibu nasi kwa habari zaidi .................................
No comments:
Post a Comment