NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Saturday, January 12, 2013

BOB JUNIOR AOA KIMYAKIMYA


Stori: Mwaija Salum na Joan Lema

KUTOKANA na ndoa hiyo kuwa ya aina yake, hivi karibuni waandishi wetu walimuweka kati Bob Junior na kumbana kwa maswali  ya “why, kwanini, ikawaje” aoe kimyakimya wakati yeye ndiye ‘prezidaa’ wa masharobaro?

Bob Junior akafunguka: “Nilifunga ndoa Desemba mwaka jana. Nililazimika kuoa kimyakimya kutokana na masharti ya wazazi wa pande zote mbili kwamba ndoa isifungwe kwa mbwembwe.”

Alisema, hata idadi ya wahudhuriaji katika ndoa hiyo ilidhibitiwa, hivyo kuruhusu ndugu na marafiki wachache kushuhudia tukio hilo.…

WOLPER AFUNGUKIA UHUSIANO WAKE NA SAJUKI

Stori:George Kayala

SIKU chache baada ya kifo cha mwigizaji Juma Kilowoko, mwigizaji Jacqueline Wolper amefungukia uhusiano wake na marehemu hadi kufikia hatua ya kuchangia kiasi cha shilingi milioni 15 kwa ajili ya matibabu.

Akizungumza na Funguka na Risasi kwenye msiba wa msanii huyo pande za Tabata Bima jijini Dar, Wolper alisema Sajuki alimpenda kama kaka yake wa damu ndiyo maana alikuwa tayari kumsaidia kwa hali na mali.
“Kila mmoja alinishangaa nilipotoa shilingi milioni 15 kwa ajili ya gharama za matibabu ya marehemu. Ukweli ni kwamba marehemu nilimpenda kama kaka yangu wa damu.” alisema Wolper huku akibubujikwa na machozi.…

JACK MAISHA PLUS, RUBI WAFANYA MAZOEZI KUONDOA ‘VITAMBI’

Stori:Gladness Mallya
MSHIRIKI wa Shindano la Maisha Plus Season II, Jacqueline Dastan ‘Jack Maisha Plus’ na shosti wake ambaye ni bosi wa Kundi la Nderemo Arts Group, Khadija Kasongo ‘Rubi’ wameanza kufanya mazoezi ya viungo kwa lengo la kuondoa ‘vitambi’.

Wasanii hao wameamua kuingia kwenye ‘tizi’ baada ya kuona vitambi vinakuwa tishio kwao, jambo ambalo limekuwa likiwakosesha raha kwani wanahisi hawana mwonekano mzuri.
Jacqueline Dastan ‘Jack Maisha Plus’.
“Tunafanya mazoezi asubuhi na…

NDIKUMANA WA UWOYA ANAUMWA

Stori: Imelda Mtema
MSAKATA kabumbu mkali nchini Rwanda ambaye pia ni mume wa diva wafi lamu za Kibongo, Irene Uwoya, Hamad Ndikumana ‘Katauti ’ ni mgonjwa kiasicha kushindwa kuendelea kuichezea timu yake ya Rayon Sports ya Rwanda.
Irene Uwoya
Akiwasiliana na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya mtandao wa kijamii wa ‘Facebook’,Ndikumana alisema kuwa kwahivi sasa hali yake siyo nzuri kiafyana ndiyo maana ameshindwa kujiunga na mazoezi ya timu yake hiyo.
“Kwa hivi sasa bado naumwa,hivyo sija ichezea timu yangu mchezo wowote mpaka afya yangu itakapo…

HILI NI DARASA HURU, KUCHUJA PENZI HALISI NA MAZOEA - 5

TUNAENDELEA na mada yetu tuliyoianza wiki kadhaa zilizopita. Yatazame maisha yako kabla hujakutana naye, halafu jiulize mabadiliko yako. Je, ni hasi au chanya?

Inawezekana kweli ameyafanya maisha yako kuwa na furaha lakini hiyo furaha anaidumisha vipi? Isije ikawa anakufurahisha pale tu anapokuwa na shida zake, pindi unapomtatulia huyo anakwenda zake, akirudi tena ujue ana shida.
Mathalan, mwenzi wako anatimiza kila kitu unachohitaji. Anageuka mtu wa ndiyo na kutekeleza kila ombi lako. Wewe unajiona unatisha kwa kuona kwamba mwenzi wako anakunyenyekea unavyotaka. Kumbe mwenzako ana malengo yake, mkishaingia faragha na kukidhi haja…

KUMBE WENYE BAA WENGI WANAZUIA JUA BADALA YA MVUA!

SIKU hizi kuna baa zinafunguliwa kwa wingi sehemu mbalimbali nchini. Ili baa iwe ya kisasa zaidi, inaezekwa kwa makuti na kushikiliwa na miti mikubwa na mirefu iliyonakshiwa.
Wateja wengi wakiona baa ipo hivyo, wanamiminika kuliko hata wanavyokwenda kwenye nyumba za ibada.

Lakini tatizo linakuja kipindi mvua inaponyesha! Baa nyingi huwa zinavuja kiasi cha kuwafanya wateja wakimbilie sehemu nyingine kujisitiri wasilowane.
Hii inaonesha kwamba, wamiliki wa baa hizo wanatumia akili zao kupambana na jua lisiwapate wateja wao na si mvua. Wamiliki hao waliangalie hilo kuanzia sasa kwani Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema mvua kubwa itaendelea kunyesha nchini mpaka mwezi Machi mwaka huu.…

No comments:

Post a Comment