Na Mwandishi Wetu
MCHUNGAJI wa Kanisa la Calnel Centre lililopo Uwanja Ndege mjini hapa,
Elias Ambakisye (pichani juu) amemuacha mkewe aitwaye Sabina Lameck kwa
madai ya ushirikina.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, tukio hilo la aina
yake lilitokea hivi karibuni katika kikao kilichohudhuriwa na familia ya
mchungaji huyo, wazee wa kanisa na waandishi wa habari kilichoitishwa
na mtumishi huyo wa Mungu.
Habari zaidi kutoka kwa chanzo chetu
zinapasha kwamba, mchungaji huyo aliitisha kikao hicho ili wahudhuriaji
wamsikie Sabina aliyekuwa mkewe kabla ya kuachana miaka minne iliyopita
akitubu mambo ya kishirikina aliyomtendea.
Imedaiwa kuwa, baada ya
mama huyo kupewa nafasi ya kutubu alianza kumtuhumu muumini wa kanisa
hilo (jina kapuni) kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na Ambakisye ambaye ni
mumewe wa ndoa.
Habari zinaongeza kuwa, Sabina aliwaeleza
wahudhuriaji wa kikao hicho kwamba mwanamke huyo alichukua nguo za
mchungaji na za kwake na kuzipeleka kwa kalumanzila zikafanyiwe ndumba
ili warudiane na mumewe.
Sabina aliongeza kuwa, jambo la kushangaza
ni kwamba baada ya kufanya ushirikina hawajarudiana na mumewe isipokuwa
imekuwa kinyume kwani Ambakisye anataka kumuoa muumini huyo.
Kwa
upande wake mchungaji huyo, alimtuhumu Sabina kwamba ni mshirikina na
kudai aliamua kutengana naye kutokana na tabia hiyo pia kuzaa na
mwanaume mwingine kitendo kilichomdhalilisha sana.
No comments:
Post a Comment