Na Gladness Mallya
MAMA
wa aliyekuwa msanii wa muziki na filamu Bongo, Hussein Ramadhan Mkieti
‘Sharo Milionea’ amefungukia gari aliloacha mwanaye pamoja na mimba
ambayo inadaiwa ni yake.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Mama Sharo alisema: “Kuhusu gari
lile Toyota Opa aliloacha marehemu mwanangu naliuza kwani siwezi
kuliendesha na haliwezi kukaa bila kufanya kazi yoyote.
“Kwa upande
wa Marry Lucas wa Sumbawanga msichana aliyejitokeza baada ya Sharo
kufariki na kusema ana ujauzito wake, siwezi kumtambua kwa sababu enzi
za uhai Sharo hakuniambia kuwa ana mchumba wala mpenzi.”
Sharo Milionea alifariki dunia Nov 26, mwaka jana kwa ajali ya gari iliyotokea mkoani Tanga.
Siku chache baadaye, Marry aliibuka na kudai alikuwa mpenzi wa Sharo na ana ujauzito wake.
No comments:
Post a Comment