WATU WAWILI WAMEFARIKI MASASI MKOANI MTWARA NA WENGINE WENGI KUJERUHIWA VIBAYA ..
Chanzo
cha vurugu zilizoanzishwa na madereva bodaboda huko Mtwara - Masasi
zinatajwa kuwa ni tukio la mwenzao aliyekuwa anakimbizwa na Polisi
kudondoka na kuumia vibaya, ikisemekana kuwa imekuwa ni tabia ya muda
mrefu ya Polisi kuwaonea kwa kuwakamata na kuwataka wawapatie kiasi cha
fedha.
Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya inatajwa kuchomwa moto, Zikiwepo Ofisi za CCM, nyumba mbili za mheshimiwa Anna Abdallah, Nyumba ya Mbunge Mariam Kasembe pamoja na Mahakama ya Mwanzo wilayani hapo.
Hadi sasa Polisi wanaendelea na jitihada kurudisha mazingira ya Amani.
Endelea kuwa karibu na EATV kwa taarifa zaidi kuhusiana na hili.
No comments:
Post a Comment