1. Wakati
ukizungumza nae, jaribu kuzungumzia "hisia" kama vile kumbu kumbu yako
ya utotoni, matarajio ya baadae au matamanio yake. Mada hii ya
mazungumzo yenu yatafungua milango ya hisia zake ghafla.
2. Wanawake
huhitaji mwanaume asiyekuwa na uoga wa kuwamiriki na kuwaongoza. Wakati
unazungumza na mwanamke tawala mazungumzo yetu, kamwe usimpe nafasi ya
yeye kuanza kufikiri, kuwa nini uchokuwa ukizungumza.
3. Kuwa
makini wakati unapokuwa ukizungumza naye kwa majibu yasiyo na anayokuwa
akikujibu, na kama kwa bahati mbaya ukonaye karibu kiasi cha kugusana,
basi jisogeze pembeni wakati ukiwa unaendelea kuongea ili asishtukie au
unaweza kumuona hayuko sawa katika utoaji majibu.. kwa kawaida
atakuonyesha ishara, hivyo kuwa nazo makini.
4. Kumbuka hii kauli mbiu "Ucheshi/vituko si mapenzi". Wanawake huvutiwa
sana na wanaume wanaoweza kuwafanya wawe na furaha muda wote. Usijikite
zaidi katika kufanya utani unaopita kiasi na kusahau ulichokuwa
unaongea. Bali jikite zaidi katika mambo yanayomfanya ajisikie kuwa na
msisimko na starehe wakati ukonae.
5. Zama katika undani wa mazungumzo baina yako na yeye. Mwanamke
huendana na mwanaume asiyekuwa muoga wa kuzungumzia mambo binafsi kwa
ukaribu.
6. Wanawake wengi hupenda kujua maoni yako kuhusiana na jinsi
unavyomuona. Mwambie vitu unavyoviona kutoka kwake, lakini jaribu kuwa
makini ili usitamke vitu vingine vitakavyo msababishia apoteze furaha.
7. Epuka kumpa ofa nyingi mwanamke, mwanamke huwa na mashaka na mwanaume
anayempatia vitu viingi kwa wakati mmoja ama kila mara. Kwasababu
atafikiri vitu unavyompatia ni kutaka kumvutia tu ili umpate kiurahisi.
Kitu ambacho baadae kitaleta madhara makubwa.
8. Kama unahitaji kujua njia nzuri ya kuweza kuongea na mwanamke au
msichana bila kumfanya asichikie au kuboreka, basi usitumie njia ya
kumuuliza maswali mengi katika mzungumzo yenu. Bali cha zaidi jaribu
kueleza mawazo yako kuhusu vitu flani.
9. Kumbuka kauli juu ya kuuliza maswali: Badala ya kumuuliza "wewe
umekulia wapi?", uliza "unaonekana kama hujakulia maeneo haya!" Hii
itakusaidia wewe kufanya uchunguzi juu yake bila yeye kujua.
10. Usifiche utambulisho wako - zungumza vitu kutoka katika hisia zako,
onyesha uhalisia wako katika kuzungumza na usitumie mikogo ya mtu
yeyote.
Njia bora ya kufikiria jinsi ya kuzungumza na mwanamke, ni kutambua njia
sahihi ya mazungumzo ya furaha na yakimahaba utakayopenda kuitumia,
usimuige mtu. Kuzungumza na mwanamke sii vigumu bali nikujua ni vitu
gani hasa mwanamke hapendi kuvizungumzia na vitu gani anapenda
kuvisikia. Fuata maelekezo hapo juu utaona matunda yake...kisha rudi
utoe maoni yako.
MUHIMU: Maelekezo haya yote yatafanikiwa kwa mwanamke mwenye kuhitaji
mapenzi ya kweli - yani sio kwa wanawake wanaolenga kuchota pesa kwako
na kutokomea. Hivyo kuwa makini sana
No comments:
Post a Comment