BRAZIL BADO INASAFARI NDEFU KUFIKIA MAFANIKIO - NEYMAR.
MSHAMBULIAJI nyota wa
kimataifa wa Brazil, Neymar amedai kuwa nchi yake ina safari ndefu kama
wanahitaji kulibakisha Kombe la Dunia nchini kwao mwaka ujao. Katika
mahojiano na vyombo vya habari mara ya timu yake kubanguliwa mabao 2-1
na Uingereza katika Uwanja wa Wembley Neymar amesema timu yake inatakiwa
iboreshe mchezo wake ili uwe wa kiushindani zaidi. Nyota
huyo ambaye anafanishwa na nguli wa zamani wa soka Pele alidai kuwa
wakiwa kama wenyeji wa michuano hiyo watakuwa katika shinikizo zaidi
lakini labda mashabiki wao wanaweza kuwasaidia kulinyakuwa kombe hilo. Brazil kwasasa imeporomoka katika viwango vya ubora vya Shirikisho la Soka Duniani-FIFA mpaka kufikia katika nafasi ya 18. Neymar
ambaye mkataba wake na klabu ya Santos unaishia mwaka 2014 pia alidai
kuwa ndoto zake wakati akiwa mdogo ni kwenda kucheza soka barani Ulaya
na kuchagua nchi za Ujerumani na Hispania kama sehemu ambapo anaweza
kwenda wakati mkataba wake utakapomalizika.
No comments:
Post a Comment