Na Khatimu Naheka
PAMOJA na mashabiki wa soka
Tanzania kutarajiwa kupata burudani ya kutosha kwenye mchezo wa kirafiki
dhidi ya Cameroon leo, viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
wamekesha kwa siku tatu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere.
Timu ya Cameroon imekuwa ikitua nchini kwa mafungu kuanzia
Jumapili usiku hadi jana mchana saa nane ambapo alitua kiungo Benoit
Assou-Ekotto.
Mshambuliaji hatari wa Cameroon, Samuel Eto’o mpaka
jana alasiri alikuwa hajatua hapa nchini na kiongozi mmoja wa juu wa TFF
pamoja na dereva walikuwa wakihaha kwa siku tatu uwanjani hapo.
Filamu
ilianza Jumapili jioni baada ya viongozi hao kuambiwa kuwa kuna baadhi
ya wachezaji pamoja na viongozi wa benchi la ufundi watatua, lakini
walipokwenda walirudi makwao usiku wa manane kutokana na kila mara
kubadilishiwa shirika la ndege.
“Wamekuwa wakielezwa kuwa Eto’o
pamoja na wachezaji wengine wanakuja saa tatu asubuhi lakini wakifika
pale wanakaa mpaka saa tano usiku bila kuambulia chochote.
“Wamekuwa
wakifika hapa na kupata baadhi ya wachezaji, lakini wakati mwingine
wanakuja saa sita mchana wanakaa mpaka usiku mnene ndiyo wanaondoka.
“Lakini
huu ujio wa Eto’o umewasumbua sana, kila wakati wanaambiwa anakuja na
ndege fulani wanakimbia kuja hapa, lakini hawaambulii chochote, jana
(juzi) wametoka hapa usiku mnene, leo tazama hadi sasa bado hawajamuona.
“Waliambiwa
anakuja asubuhi, wamefika hapa mapema sana na sasa ni alasiri
wanaondoka na bado hawajaambulia kitu, nasikia wameambiwa waje hapa
usiku saa tano,” kilisema chanzo.
No comments:
Post a Comment