NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Monday, February 25, 2013

ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’ BACK TO SCHOOL

AJIPANGA KURUDI DARASANI UPYA!
Ni takriban mwezi mmoja tangu staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ au ‘Lizy’ alipopata dhamana na kurejea uraiani akiwa amesota katika mahabusu ya Gereza la Segerea, Dar karibia miezi kumi, akikabiliwa na shitaka la kumuua bila kusudia mwigizaji Steven Kanumba.

BACK TO SCHOOL
Akiwa uraiani akisubiri kesi yake kuendelea kuunguruma, Lulu sasa anajipanga kurejea darasani kujiendeleza na masomo (back to school) kwa mara nyingine.
Habari za ndani zilieleza kuwa lengo ni kumwezesha staa huyo mkali mbele ya kamera za Bongo Movies kupambana na changamoto za kimaisha.
Habari hizo za uhakika zilieleza kuwa Lulu yupo kwenye mchakato wa kurudi shule ili aweze kuendelea na masomo ya sekondari aliyokuwa amesimama kwa muda.
AKWAMA, KISA?
Pamoja na kwamba mkakati huo unaendeshwa na familia, habari hizo zilidai kuwa suala kubwa linalokwamisha program hiyo kwa sasa ni kipato.
Habari za chini zilidai kuwa familia kwa sasa haina uwezo wa kumlipia shule za gharama kubwa na badala yake anatakiwa kuanza kufanya kazi ili ajikwamue katika hilo.
KUCHANGAMKIA TENDA ZA FILAMU
Ilifahamika kuwa kazi ambazo zitamwingizia mkwanja mrefu ili kumudu gharama za masomo yake na mdogo wake kama ilivyokuwa awali ni kuchangamkia tenda za filamu kutoka kwa watu mbalimbali ambazo kwa bahati nzuri tayari zimejitokeza.
Pia ilifahamika kuwa mbali na kusoma na kusomesha, alikuwa akilipa kodi ya nyumba na mambo mengine ya kifamilia hivyo atarejea kule kwa awali.
NENO LA DK. CHENI
Kwa mujibu wa mwigizaji mkubwa ambaye ni mtu wa karibu wa familia ya Lulu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’, kurudi shuleni kwa staa huyo ni jambo jema ili aweze kujikwamua kielimu na kupambana na maisha ili kufanikisha malengo aliyojipangia.
Hakuna ubishi kuwa kurejea darasani kwa Lulu ambaye bado ni mdogo kiumri ni nafasi pekee ya kufanikisha malengo yake hata kama ni sanaa ambaye akishapata elimu ataifanya kisomi zaidi.
KWA NINI ALIACHA SHULE?
Kabla ya kukutwa na mashaibu, Lulu alipitia shule mbalimbali za sekondari kabla ya kusimama kumaliza au kuacha masomo akiwa kidato cha nne katika Sekondari ya Perfect Vision iliyopo Ubungo, Dar lakini sababu za kufanya hivyo hazikupatikana.

No comments:

Post a Comment