AJIPANGA KURUDI DARASANI UPYA!
Ni takriban mwezi mmoja tangu staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth
Michael ‘Lulu’ au ‘Lizy’ alipopata dhamana na kurejea uraiani akiwa
amesota katika mahabusu ya Gereza la Segerea, Dar karibia miezi kumi,
akikabiliwa na shitaka la kumuua bila kusudia mwigizaji Steven Kanumba.
BACK TO SCHOOL
Akiwa uraiani akisubiri kesi yake
kuendelea kuunguruma, Lulu sasa anajipanga kurejea darasani kujiendeleza
na masomo (back to school) kwa mara nyingine.
Habari za ndani
zilieleza kuwa lengo ni kumwezesha staa huyo mkali mbele ya kamera za
Bongo Movies kupambana na changamoto za kimaisha.
Habari hizo za
uhakika zilieleza kuwa Lulu yupo kwenye mchakato wa kurudi shule ili
aweze kuendelea na masomo ya sekondari aliyokuwa amesimama kwa muda.
AKWAMA, KISA?
Pamoja na kwamba mkakati huo
unaendeshwa na familia, habari hizo zilidai kuwa suala kubwa
linalokwamisha program hiyo kwa sasa ni kipato.
Habari za chini
zilidai kuwa familia kwa sasa haina uwezo wa kumlipia shule za gharama
kubwa na badala yake anatakiwa kuanza kufanya kazi ili ajikwamue katika
hilo.
KUCHANGAMKIA TENDA ZA FILAMU
Ilifahamika kuwa
kazi ambazo zitamwingizia mkwanja mrefu ili kumudu gharama za masomo
yake na mdogo wake kama ilivyokuwa awali ni kuchangamkia tenda za filamu
kutoka kwa watu mbalimbali ambazo kwa bahati nzuri tayari zimejitokeza.
Pia
ilifahamika kuwa mbali na kusoma na kusomesha, alikuwa akilipa kodi ya
nyumba na mambo mengine ya kifamilia hivyo atarejea kule kwa awali.
NENO LA DK. CHENI
Kwa mujibu wa mwigizaji mkubwa
ambaye ni mtu wa karibu wa familia ya Lulu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’,
kurudi shuleni kwa staa huyo ni jambo jema ili aweze kujikwamua kielimu
na kupambana na maisha ili kufanikisha malengo aliyojipangia.
Hakuna
ubishi kuwa kurejea darasani kwa Lulu ambaye bado ni mdogo kiumri ni
nafasi pekee ya kufanikisha malengo yake hata kama ni sanaa ambaye
akishapata elimu ataifanya kisomi zaidi.
KWA NINI ALIACHA SHULE?
Kabla ya kukutwa na
mashaibu, Lulu alipitia shule mbalimbali za sekondari kabla ya kusimama
kumaliza au kuacha masomo akiwa kidato cha nne katika Sekondari ya
Perfect Vision iliyopo Ubungo, Dar lakini sababu za kufanya hivyo
hazikupatikana.
No comments:
Post a Comment