UPENDO
ndiyo dini yangu! Ndiyo maana natumia safu hii kuwarekebisha mastaa
wetu ili nitii matakwa ya dini yangu yaani kuwapenda! Hakuna ubishi kuwa
umaarufu ni gharama. Ni ghali. Wakati mwingine husababisha kubadili
maisha halisi ili kufikia lengo. Ikiwezekana kuondoa utu kwa kujitoa
fahamu na kufanya mambo ya kujidhalilisha. Ndivyo ilivyo kwa wasanii
wetu. Imewabidi kuishi maisha ya kuigiza ili kujitwalia umaarufu.
Ili kupata umaarufu ni lazima uwe na fedha. Itakubidi ujue sehemu za
kwenda kubadilisha mawazo na kustarehe na mastaa wenzako. Siyo sehemu za
bei rahisi. Mara nyingi kama staa akijishusha sana, ni kwenye migahawa
kama ile ya pale Mlimani City, Dar.
Hawali vyakula vya ovyo. Ni baga
na ‘take away’ za gharama. Siyo chipsi vumbi. Hawapandi usafiri wa
jumuiya (public transport). Unachezea ustaa wewe?
Ili kukidhi
matakwa tajwa hapo juu uitwe staa inawalazimu kutafuta fedha kwa njia
yoyote ile ili kugharamia ustaa. Hilo ndilo lililowaponza mastaa wa kike
Bongo. Kwa kuwa hawana vipato na wanahitaji maisha ya kujiachia kwenye
kumbi za starehe usiku na kulala mchana kutwa, imewabidi kutumia miili
yao. Ni kwa kujiuza na kuuzwa kwa wanaume kutoa huduma ya ngono ili
kujipatia fedha za kushikilia ustaa. Ama kweli kusaka umaarufu
kumewafanya dada zetu kuwa watumwa wa ngono.
Ipo mifano lukuki kwa
mastaa walioamua kuwaacha wanaume waliokuwa nao kabla hawajapata
umaarufu na kukimbilia kuolewa na watu wenye fedha.
Hata hivyo, kwa kuwa walifuata fedha na siyo mapenzi kwa wanaume hao, walipoishiwa na mapenzi yaliisha. Ndoa ziliota mbawa.
Wapo mastaa wa kike walioshindwa kudumu kwenye ndoa kwa kuwa wanaume waliowaoa waliishiwa na pesa.
Iko wapi ndoa ya kifahari ya Irene Uwoya? Kuna madai kuwa baada ya
mumewe Hamad Ndikumana ‘Kataut’ kuishiwa fedha, ndipo dada yetu
akazingua.
Unakumbuka ndoa ya kifahari ya Jacqueline Patrick na
Abdullatif Fundikira? Ilielezwa kuwa baada ya jamaa huyo kutupwa selo
katika Gereza la Keko, Dar kwa kisanga cha mihadarati, Jack alichukua
hamsini zake, akijua kabisa kwamba mkwanja umeota mbawa. Hakuwahi kwenda
kumuona selo kudhihirisha kuwa hakuwa na mapenzi ya dhati na mumewe
huyo bali alifuata mkwanja.
Unakumbuka penzi la Jacqueline Wolper na
Abdallah Mtoro ‘Dallas’? Inasadikiwa kuwa baada ya fedha za mshikaji
huyo aliyekuwa amemnunulia Wolper gari aina ya BMW X6 kurudi kwao ndipo
sistaduu huyo akakata mguu na kusitisha uchumba wao.
Unajua anayempa
Wema jeuri ya kubadili magari kama nguo, kutamba kununua nyumba ya
mamilioni na kufungua ofisi ya kifahari? Inaelezwa kuwa ni mume wa mtu
anayetajwa kwa jina la Clement au CK, kigogo katika idara nyeti nchini.
Aunt Ezekiel ameolewa na Sunday Demonte, jamaa mwenye mkwanja mbuzi
ambaye hata hivyo hawaishi wote. Aunt yupo Bongo akisubiri kutumiwa
fedha ya matumizi na bwana huyo aliyeko Dubai.
Hivi karibuni
Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ alinaswa na mapaparazi wa Global akiuzwa
kwa dola 500 akafanye ngono na mwanaume aliyejifanya Mtanzania aishie
Marekani. Ni aibu lakini atafanyaje ili kukidhi vigezo vya ustaa? Lazima
awe na fedha kwa njia yoyote. Ipi? Kukubali kuuzwa kingono.
Nimetoa
mifano michache mno lakini ni mingi. Ukweli ni kwamba hali ni mbaya.
Wasipobadilika, wataendelea kudhalilika sana tu kabla ya madhara mengine
ikiwemo kuambukizwa magonjwa hatarishi hasa Ukimwi. For the love of
game!
No comments:
Post a Comment