Kwa
kumalizia uchambuzi wa kundi la kwanza ambalo nilieleza kuwa linaundwa
na wanawake wenye umri mdogo ambao hupenda wanaume kutokana na
muonekano, vema nitaje bahati mbaya ambazo wanaweza kukutana
nazo.Wanawake wa kundi hili huwa na bahati mbaya moja kubwa ambayo ni
kusalitiwa na wanaume.
Sababu ni kuwa wanaume hao mara nyingi
hutawaliwa na kiburi kwamba wao ni wazuri na wanapendwa, kwa hiyo hukosa
msimamo na utulivu wa kweli.
Kwa
vile hupenda kulelewa, hutoka na wanawake wengine ambao wataonekana
wana fedha zaidi. Kadhalika, hujiona wao ni tabaka maalum sana, kwa hiyo
huwa wanataka wanyenyekewe hata kama ni kwa jambo ambalo linawahitaji
kunyenyekea.
Wenye tabia ya kupenda wanaume kutokana na muonekano wapo wengi, kwa
hiyo unaweza kupenda kesho yake asubuhi mwingine naye akamtaka mwanaume
huyohuyo wa kwako, hivyo kuleta ushindani wa kimaslahi kati ya mwanamke
mmoja na mwingine.
Tafsiri ya jumla ni kwamba wanaume ambao humulikwa na wanawake wa
kundi hili, aghalabu huwa siyo waaminifu. Kutokana na hali hiyo,
wanawake hao mara nyingi husumbuliwa na mateso ya mapenzi, wakilalamikia
jinsi wanavyotendwa au wasivyo na bahati ya kupendwa.
KUNDI LA PILI
Kwa kawaida, kundi hili halina tabaka la umri. Wanaounda kundi hili
wanaweza kuwa wasichana wadogo au hata wanawake watu wazima. Kipaumbele
chao siku zote huwa ni kupata wanaume ambao watawalea, yaani
watakaokidhi haja zao.
Wanaweza kuangukia hata kwa wanaume wasiowapenda ilimradi wapate
unafuu wa kuishi vizuri. Wao huwa hawana kile kitu kinachoitwa ‘mapenzi
ya dhati kutoka moyoni’, isipokuwa hujenga mazoea mpaka huhisi wanapenda
au wanapendwa.
Kutokana na ukweli huo kwamba huwa hawazingatii mapenzi ya dhati
kutoka moyoni, wanawake wanaounda kundi hili huwa hawachagui umri wa
wanaume. Iwe ni kwa vijana wadogo mpaka wazee wenye umri sawa na
vikongwe.
Mrembo mwenye umri wa miaka 24, anapoingia kwenye uhusiano wa
kimapenzi na mzee mwenye umri wa miaka 70 ambaye kiuhalisia ni babu
yake, hilo haliwezi kuwa jambo geni, isipokuwa kilichozingatiwa na
mwanamke husika ni unafuu wa kuishi.
Wanawake wa kundi hili, hushawishika kutokana na jinsi
wanavyopokelewa na wanaume. Namna ambavyo mwanaume anavyowajibika katika
utoaji wa huduma za kimsingi na hata za ziada kwa mwanamke wa kundi
hili, humfanya apate alama nyingi za ushindi.
Itaendelea wiki ijayo.
No comments:
Post a Comment