Stori: Musa Mateja
KIJANA
aliyejipatia umaarufu kwa kumvamia msukuma kambumbu wa Real Madrid,
‘Kaka’, Nagari Kombo amedaiwa kuwa ndiye anayemiliki penzi la Mbongo
Fleva, Estalina Sanga ‘Linnah’.
Kwa
mujibu wa chanzo makini, wawili hao wamekuwa wakionekana kwenye viwanja
tofauti vya starehe na mara kwa mara wamekuwa wakishea vitu vyao
ikiwamo gari la Linnah.
“Mbona siyo siri, Linnah na Nagari ni wapenzi kitambo na siku hizi
wanajiachia bila kificho kwa raha zao. Hawamuogopi mtu,” kilisema chanzo
hicho kilichoomba hifadhi ya jina lake.
Paparazi wetu alipomtafuta Linnah kuhusiana na ishu hiyo, alipokea
simu na alipoulizwa kinachoendelea baina yao alikata simu fasta na
kuizima kabisa.
No comments:
Post a Comment