
Niaje mpenzi msomaji wangu? Kama ilivyo kawaida ya safu hii, inakukutanisha na mastaa mbalimbali ambao wamejaliwa kupata watoto na kuongea kuhusu masuala ya familia.


Shamsa: Nzuri, karibu sana.
Amani: Mbona umenawiri hivyo, ni ulezi tu?
Shamsa: Mambo ya saluni haya, si unajua mwanamke urembo!

Shamsa: Mwenzangu maana hapa unavyotuona, vitu vya kuvunjika inabidi tuvihamishe manaa ni mtundu balaa.
Amani: Unajisikiaje unavyomuona amekuwa hivi?
Shamsa: Dah! Kiukweli siwezi hata kuelezea furaha yangu. Nafurahi sana kuitwa mama.
Amani: Niambie ulijisikiaje siku ya kwanza pale ‘Leba’ ulipoambiwa umepata mtoto wa kiume?
Shamsa: Jamani sikuweza kusema zaidi ya kulia tu yaani huyu mtoto aliniliza sana.
Amani: Kwa nini sasa?

Amani: Kwa kipindi kirefu ulipotea, je ilisababishwa na ulezi nini?
Shamsa: Kweli, niliamua kumlea mtoto wangu kwanza lakini kwa hivi sasa nimerudi upya kwenye sanaa.
Amani: Kutokana na kuzaa, huoni kama utakuwa umeharibu umbo lako?

Amani: Ni nani ungependa kumshukuru zaidi kwa ajili ya mtoto wako?
Shamsa: Wa kwanza kabisa ni baba yake na Zamaradi ambaye ndiyo alikuwa na mimi mwanzo hadi mwisho wakati wa kujifungua.
Amani: Nakushukuru sana Shamsa, acha nirudi ofisini nikawajibike.
Shamsa: Karibu tena siku nyingine.
No comments:
Post a Comment