Stori ndani ya area 255 na 254
zimebeba mitaa kwamba mwigizaji Wema Sepetu ambae aliwahi kuwa Miss
Tanzania amechukua fomu za kushiriki kwenye shindano la BIG BROTHER
2013.
Wema ameongea Exclusive kwenye
AMPLIFAYA ya CLOUDS FM na kusema ameshangaa hata yeye kujiona yuko kila
sehemu akizungumziwa kwamba anashiriki.
Ukweli ni kwamba bado
hajachukua fomu ya kushiriki na wala hajawa na mpango wa kwenda BBA 2013
kwa sababu ana mipango mingi ikiwemo kufungua ofisi yake mpya.
Lakini kwenye line nyingine
Wema kasema anafurahi kusikia watu wakimuongelea hivyo kwa sababu
wameonyesha kumuamini kwa kumuona anaweza kuingia BBA, anachosisitiza ni
kwamba aliwahi kuwaza kwenda BBA lakini hajawa na uhakika kuhusu yeye
kushiriki.
No comments:
Post a Comment