KATIKA kile kilichotafsiriwa kuwa ni kuwafutilia mbali wasanii wenzake, Blandina Chagula na Ruth Suka ‘Mainda’ aliowahi kudaiwa kutoka nao kimapenzi, staa wa filamu Bongo, Vincent Kigosi amefunguka kuwa, hatarajii kuoa msanii kwani anaogopa presha.
Vincent Kigosi.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Ray alisema kuwa anajua matatizo
ya kuoa staa hivyo ili kuepukana nayo ameamua kuwekeza penzi lake kwa
mwanamke anayefanya kazi benki (jina amelihifadhi kwa sasa) akidai kuwa
huyo ndiye tulizo la moyo wake.
Ruth Suka ‘Mainda’.
“Kaa ukijua kuwa sina mpango wa kumuoa staa
yeyote, mwanamke ninayetarajia kumuoa ni mfanyakazi wa benki na mipango
yangu ikikamilika nitakueleza kila kitu. Mimi sitaki presha bwana,”
alisema Ray.
No comments:
Post a Comment