MESSI KUMALIZIA SOKA LAKE ARGENTINA.
MSHAMBULIAJI nyota wa
Barcelona, Lionel Messi amedokeza kuwa anaweza kumalizia soka nchini
Argentina baada ya kuongeza mkataba na Barcelona ambao utaishia June
2018. Mshambuliaji
huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 25 ambaye ameongeza
mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo, alifanikiwa kuvunja rekodi ya
kufunga mabao mengi zaidi mpaka kufikisha mabao 91 mwaka jana kwa klabu
na nchi yake. Akizungumza
na tovuti ya klabu hiyo Messi amesisitiza kuwa alikuwa akitaka
kumalizia soka barani Ulaya akiwa na Barcelona na hajafikiria kwenda
katika klabu yoyote barani humo pindi mkataba wake utapokwisha. Messi
alisaini mkataba wake mpya Alhamisi mchana na kuwafuata beki wa timu
hiyo Carles Puyol na Xavi Hernandez ambao wote waliongeza mikataba yao
mwezi uliopita ambayo itawaweka Camp Nou mpaka 2016. Shughuli
za utiaji saini mkataba huo mpya zilihudhuriwa na rais wa Barcelona
Sandro Rossel, makamu wa rais Josep Maria Bartomeu na mkurugenzi wa
michezo wa klabu hiyo Andoni Zubizarreta.
No comments:
Post a Comment