NEMAYAN
ROBERT
- THE HOODS SPICK
Friday, February 8, 2013
UEFA YAPUNGUZA GHARAMA ZA TIKETI ZA FAINALI CHAMPIONS LEAGUE.
SHIRIKISHO la Soka
barani Ulaya-UEFA limejibu hoja ambayo ilikuwa ikikua kuhusiana na
gharama kubwa za kutizama mechi nchi Uingereza kwa kushusha bei ya
tiketi za fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa mpaka kufikia paundi
68. UEFA
walituhumiwa kuwanyonya mashabiki wakati wa mchezo wa fainali ya
michuano hiyo uliochezwa miaka miwili iliyopita ambapo Barcelona
iliifunga Manchester United kwa mabao 3-1 kwa kuwalipisha paundi 176 kwa
tiketi ya bei rahisi. UEFA
ilitangaza kuwa imesikiliza vilio vya mashabiki na kuamua kupunguza bei
ya tiketi kwa ajili ya mchezo huo wa fainali utakaochezwa Mei 25 mwaka
huu baada ya kupata maoni kutoka kwa mashabiki wa soka sehemu mbalimbali
barani Ulaya. Tiketi
13,000 kati ya 59,000 zitakazouzwa ndio zitapata punguzo la bei hizo
mpya lakini zilizobakia zote zitauzwa kwa gharama za juu zitakazoanzia
paundi 140 mpaka 330.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment