NEMAYAN

NEMAYAN

ROBERT

  • THE HOODS SPICK

Monday, February 25, 2013

MASTAA WA KIKE BONGO; KUTAFUTA USTAA, FEDHA KUTAWADHALILISHA SANA TU!

UPENDO ndiyo dini yangu! Ndiyo maana natumia safu hii kuwarekebisha mastaa wetu ili nitii matakwa ya dini yangu yaani kuwapenda! Hakuna ubishi kuwa umaarufu ni gharama. Ni ghali. Wakati mwingine husababisha kubadili maisha halisi ili kufikia lengo. Ikiwezekana kuondoa utu kwa kujitoa fahamu na kufanya mambo ya kujidhalilisha. Ndivyo ilivyo kwa wasanii wetu. Imewabidi kuishi maisha ya kuigiza ili kujitwalia umaarufu.
Aunt Ezekiel.
Ili kupata umaarufu ni lazima uwe na fedha. Itakubidi ujue sehemu za kwenda kubadilisha mawazo na kustarehe na mastaa wenzako. Siyo sehemu za bei rahisi. Mara nyingi kama staa akijishusha sana, ni kwenye migahawa kama ile ya pale Mlimani City, Dar.
Hawali vyakula vya ovyo. Ni baga na ‘take away’ za gharama. Siyo chipsi vumbi. Hawapandi usafiri wa jumuiya (public transport). Unachezea ustaa wewe?
Ili kukidhi matakwa tajwa hapo juu uitwe staa inawalazimu kutafuta fedha kwa njia yoyote ile ili kugharamia ustaa. Hilo ndilo lililowaponza mastaa wa kike Bongo. Kwa kuwa hawana vipato na wanahitaji maisha ya kujiachia kwenye kumbi za starehe usiku na kulala mchana kutwa, imewabidi kutumia miili yao. Ni kwa kujiuza na kuuzwa kwa wanaume kutoa huduma ya ngono ili kujipatia fedha za kushikilia ustaa. Ama kweli kusaka umaarufu kumewafanya dada zetu kuwa watumwa wa ngono.
Ipo mifano lukuki kwa mastaa walioamua kuwaacha wanaume waliokuwa nao kabla hawajapata umaarufu na kukimbilia kuolewa na watu wenye fedha.
Wolper.
Hata hivyo, kwa kuwa walifuata fedha na siyo mapenzi kwa wanaume hao, walipoishiwa na mapenzi yaliisha. Ndoa ziliota mbawa.
Wapo mastaa wa kike walioshindwa kudumu kwenye ndoa kwa kuwa wanaume waliowaoa waliishiwa na pesa.
Iko wapi ndoa ya kifahari ya Irene Uwoya? Kuna madai kuwa baada ya mumewe Hamad Ndikumana ‘Kataut’ kuishiwa fedha, ndipo dada yetu akazingua.
Unakumbuka ndoa ya kifahari ya Jacqueline Patrick na Abdullatif Fundikira? Ilielezwa kuwa baada ya jamaa huyo kutupwa selo katika Gereza la Keko, Dar kwa kisanga cha mihadarati, Jack alichukua hamsini zake, akijua kabisa kwamba mkwanja umeota mbawa. Hakuwahi kwenda kumuona selo kudhihirisha kuwa hakuwa na mapenzi ya dhati na mumewe huyo bali alifuata mkwanja.
Unakumbuka penzi la Jacqueline Wolper na Abdallah Mtoro ‘Dallas’? Inasadikiwa kuwa baada ya fedha za mshikaji huyo aliyekuwa amemnunulia Wolper gari aina ya BMW X6 kurudi kwao ndipo sistaduu huyo akakata mguu na kusitisha uchumba wao.
Unajua anayempa Wema jeuri ya kubadili magari kama nguo, kutamba kununua nyumba ya mamilioni na kufungua ofisi ya kifahari? Inaelezwa kuwa ni mume wa mtu anayetajwa kwa jina la Clement au CK, kigogo katika idara nyeti nchini.
Aunt Ezekiel ameolewa na Sunday Demonte, jamaa mwenye mkwanja mbuzi ambaye hata hivyo hawaishi wote. Aunt yupo Bongo akisubiri kutumiwa fedha ya matumizi na bwana huyo aliyeko Dubai.
Hivi karibuni Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ alinaswa na mapaparazi wa Global akiuzwa kwa dola 500 akafanye ngono na mwanaume aliyejifanya Mtanzania aishie Marekani. Ni aibu lakini atafanyaje ili kukidhi vigezo vya ustaa? Lazima awe na fedha kwa njia yoyote. Ipi? Kukubali kuuzwa kingono.
Nimetoa mifano michache mno lakini ni mingi. Ukweli ni kwamba hali ni mbaya. Wasipobadilika, wataendelea kudhalilika sana tu kabla ya madhara mengine ikiwemo kuambukizwa magonjwa hatarishi hasa Ukimwi. For the love of game!

ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’ BACK TO SCHOOL

AJIPANGA KURUDI DARASANI UPYA!
Ni takriban mwezi mmoja tangu staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ au ‘Lizy’ alipopata dhamana na kurejea uraiani akiwa amesota katika mahabusu ya Gereza la Segerea, Dar karibia miezi kumi, akikabiliwa na shitaka la kumuua bila kusudia mwigizaji Steven Kanumba.

BACK TO SCHOOL
Akiwa uraiani akisubiri kesi yake kuendelea kuunguruma, Lulu sasa anajipanga kurejea darasani kujiendeleza na masomo (back to school) kwa mara nyingine.
Habari za ndani zilieleza kuwa lengo ni kumwezesha staa huyo mkali mbele ya kamera za Bongo Movies kupambana na changamoto za kimaisha.
Habari hizo za uhakika zilieleza kuwa Lulu yupo kwenye mchakato wa kurudi shule ili aweze kuendelea na masomo ya sekondari aliyokuwa amesimama kwa muda.
AKWAMA, KISA?
Pamoja na kwamba mkakati huo unaendeshwa na familia, habari hizo zilidai kuwa suala kubwa linalokwamisha program hiyo kwa sasa ni kipato.
Habari za chini zilidai kuwa familia kwa sasa haina uwezo wa kumlipia shule za gharama kubwa na badala yake anatakiwa kuanza kufanya kazi ili ajikwamue katika hilo.
KUCHANGAMKIA TENDA ZA FILAMU
Ilifahamika kuwa kazi ambazo zitamwingizia mkwanja mrefu ili kumudu gharama za masomo yake na mdogo wake kama ilivyokuwa awali ni kuchangamkia tenda za filamu kutoka kwa watu mbalimbali ambazo kwa bahati nzuri tayari zimejitokeza.
Pia ilifahamika kuwa mbali na kusoma na kusomesha, alikuwa akilipa kodi ya nyumba na mambo mengine ya kifamilia hivyo atarejea kule kwa awali.
NENO LA DK. CHENI
Kwa mujibu wa mwigizaji mkubwa ambaye ni mtu wa karibu wa familia ya Lulu, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’, kurudi shuleni kwa staa huyo ni jambo jema ili aweze kujikwamua kielimu na kupambana na maisha ili kufanikisha malengo aliyojipangia.
Hakuna ubishi kuwa kurejea darasani kwa Lulu ambaye bado ni mdogo kiumri ni nafasi pekee ya kufanikisha malengo yake hata kama ni sanaa ambaye akishapata elimu ataifanya kisomi zaidi.
KWA NINI ALIACHA SHULE?
Kabla ya kukutwa na mashaibu, Lulu alipitia shule mbalimbali za sekondari kabla ya kusimama kumaliza au kuacha masomo akiwa kidato cha nne katika Sekondari ya Perfect Vision iliyopo Ubungo, Dar lakini sababu za kufanya hivyo hazikupatikana.

RAY AKONGOROKA


Stori: Musa Mateja na Imelda Mtema
MWIGIZAJI Vincent Kigosi ‘Ray’ amezua hofu kwa ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wake baada ya kukongoroka ghafla akihisiwa anaumwa, Ijumaa Wikienda limemfuatilia hatua kwa hatua.
Vincent Kigosi ‘Ray’ alivyo kwa sasa.
KWENYE ‘BETHIDEI’ YA BATULI
Wiki kadhaa zilizopita paparazi wetu alishtuka alipomuona Ray kwenye ‘bethidei’ ya mwigizaji sistaduu Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ ndani ya Hoteli ya Shamoll iliyopo Sinza ya Lion, Dar akiwa amekongoroka na kuibua maswali kwa wahudhuriaji.
Akiwa ukumbini hapo, minong’ono ilienea kuwa Ray alionekana kukondeana katika kipindi kifupi huku baadhi ya watu wakisikika wakiulizana kulikoni kwani alikuwa meza moja na bonge la mtu, Jacob Steven ‘JB’ hivyo kumfanya kuonekana mdogo mno.
Vincent Kigosi ‘Ray’ alivyokuwa mwaka jana.
VIWANJA VYA LEADERS
Akiwa kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni, Dar wiki iliyopita, Ray aliibua mshtuko kwa mara nyingine hadi jamaa mmoja anayedhaniwa kutokuwa vizuri kichwani kumfuata na kumuwakia akimuuliza kwa hasira kuwa kulikoni akondeana kiasi hicho.
UZINDUZI WA WEMA
Kwa mara nyingine, Ray alizua hofu alipohudhuria kwenye uzinduzi wa ofisi ya Wema Sepetu uliofanyika maeneo ya Kinondoni, Dar ambapo alipoingia watu walipigwa butwaa wakimtazama na wengine kumuonea huruma wakidhani anaumwa.
IJUMAA WIKIENDA LATAKA MAJIBU
Kwa nyakati tofauti, wanahabari wetu walizungumza na Ray ambaye alitoa majibu ya kukinzana na kuzidi kutia shaka.
Ray alimwambia mmoja wa waandishi wetu kuwa kilichosababisha akongoroke kiasi hicho ni mazoezi makali anayofanya ili kupunguza unene.
Katika majibu mengine kwa mwandishi wetu mwingine, Ray alidai kuwa anafanya ‘dayati’ ikielezwa kuwa ikishafika saa 11:00 jioni ndiyo mwisho wake wa kula msosi lengo likiwa ni kupunguza mwili uliokuwa umefumuka.
Kama mtu alimuona Ray kwenye Matamasha ya Serengeti Fiesta mwishoni mwa mwaka jana, akikutana naye lazima amtazame mara mbilimbili hivyo Ijumaa Wikienda lipo mzigoni kutafuta undani wa madai kuwa huenda staa huyo mkubwa anaumwa kufuatia majibu tofauti aliyoyatoa.

Friday, February 22, 2013

KUHUSU MWANAFUNZI ALIEJIUA BAADA YA MATOKEO YA FORM IV, NA UJUMBE ALIOACHA VIKO HAPA


Tabora.
Ni kifo ambacho kimetokana na mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kanyenye Tabora Michael Fidelis kutofurahishwa na matokeo yake ya kidato cha nne yaliyotoka mwaka huu.
Kaka wa marehemu amesema “tangu jana saa 11 marehemu alikua hai kuna mwanafunzi mwingine yuko Mbeya akampigia simu kwamba akaangalie matokeo yametoka ilikua saa 11 jioni, kukuta matokeo mabaya hakurudi nyumbani akaenda anapolala ambako alipangiwa chumba kwa ajili ya kujisomea karibu na nyumbani na kuamua kuchukua uamuzi kama huu, ilikua saa tatu usiku na tumekuja kugundua saa nne baada ya yeye na mwenzake kutotokea nyumbani kuja kula”
Ameendelea kwa kusema “alijinyonga kwa kamba ya manila, ujumbe alioacha ulikua unaishilizia ukisema… mama mimi nakupenda, nimejinyonga kwa sababu matokeo ya form four sio mazuri…… mpaka sasa mwili wa marehemu umeenda kuzikwa kijijini”
Kwenye sentensi hii namkariri rafiki wa marehemu akisema “tulianza nae wote form one pale Kanyenye mpaka form IV, alikua anajitahidi sana kwenye masomo tulikua tunakwenda nae hata tution, darasani alikua mzuri tu tumeenda nae hivyo hivyo mpaka tukafanya mtihani wa form II tukafaulu wote mpaka Mock ya form IV akaja akafanya vizuri, alikua hana vurugu kwa walimu na kuhusu matokeo yalivyotoka mchana alikua kwa mama yake pale anafanya kazi, alikua anaonekana kama mtu ambae hajaelewa matokeo kwani alivyofanya mtihani alikua ana uhakika kabisa kwamba anafaulu lakini matokeo yalivyotoka yalikua tofauti kabisa”

Monday, February 18, 2013

MASTAA WA BONGO; NANI MSHIRIKINA, NANI SI MSHIRIKINA?


SIKATAI kuwa kuna uchawi au wachawi na ushirikina au washirikina. Pia sibishi kuwa kuna ulimwengu wa giza kwani hata vitabu vitakatifu vinasema kwamba kulikuwa na uchawi, wachawi, ushirikina na washirikina. Kama wewe ni msomaji wa vitabu hivyo, unakumbuka enzi za Musa katika Biblia kwenye Agano la Kale?
Continued after the jump ....


Wema.
Mbali na vitabu vitakatifu, mara kadhaa tumesikia habari za wenzetu walioendelea kuwa mambo hayo yapo na yanafanyika.
Turudi nyumbani Bongo. Katika habari zilizovuta hisia za wengi wiki iliyopita ni sakata la uchawi na ushirikina kutajwa mara nyingi zaidi katika ulimwengu wa mastaa wa Kibongo.
Nitakupa hadidu za rejea za listi ya mastaa wa Kibongo waliowahi kulalamikia ishu hiyo halafu nitafungua mjadala huru ambao utalenga kutafuta majibu sahihi ya ushirikina katika sanaa ya Kitanzania.
Huko nyuma mastaa kadhaa waliwahi kulalamika kuwa kuna watu wanawaloga. Mfalme wa TAKEU, Nice Lucas Mkenda aliwahi kulalamikiwa na mwigizaji Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ kuwa anamloga kipindi kile wakiwa na uhusiano wa kimapenzi. Swali; alikuwa anamloga ili iweje?
Mara kadhaa lejendari wa Bongo Fleva, Aboubakar Katwila ‘Q-Chillah’ amekuwa akilalamika kulogwa, huko nyuma aliwahi kukaririwa akisema kuwa alilogwa na lejendari mwenzake, Khaleed Mohamed ‘TID’. Wiki iliyopita aliibuka tena na kudai kuwa kuna msanii wa muziki huo anatumia nyota yake kufanya vizuri kwenye gemu, madai ambayo yalielekezwa kwa jamaa anayeng’ara kwa sasa, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Tukimwacha Chillah, sakata lingine linamhusu Diamond ambapo jamaa mmoja aitwaye Ustadhi Yahya Michael hivi karibuni aliibuka na kudai kuwa yeye ndiye mganga wa msanii huyo na amekuwa akimsaidia kwa muda mrefu ili kumfanya awe na mvuto na kuwa juu kimuziki huku staa huyo akishindwa kukanusha au kufafanua uhusiano wake na jamaa huyo.
Alipoulizwa msanii mwenzake, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ kuwa yeye na Diamond wamekuwa wakihusishwa na ushirikina katika muziki alikataa katakata akidai kuwa hajui chochote.
Baadaye TID naye alifunguka kuwa siyo siri kwamba aina ya muziki wanaoufanya umejaa ushirikina na kwa sasa si jambo la siri.
Itakumbukwa mwaka jana, prodyuza mkubwa ambaye ni bosi wa Studio na Lebo ya Bongo Records, Paul Khalfan Matthysse ‘P-Funk’ au Majani, naye alikiri muziki wa Bongo Fleva kujaa vitendo vya kishirikina bila kutaja nani anamloga nani na kwa malengo gani.
Bila kumsahau Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye kwa sasa hasikiki kutokana na matatizo ya kiafya, mara kadhaa aliwahi kukaririwa akidai kwamba anahisi kuna mtu anamloga.
Tukiacha upande wa muziki, kwenye filamu za Kibongo, huko ndiyo hali ni mbaya kabisa. Baadhi ya wasanii wamekuwa wakitajwa kujihusisha na masuala hayo waziwazi.
Mwaka jana, mama wa Wema Sepetu, Mariam Sepetu alikaririwa na kituo kimoja cha runinga akidai kuwa mwanaye (Wema) ameharibikiwa kwa sababu ya kufanyiwa mambo ya kishirikina na marafiki zake ndiyo maana mambo yake yanavurugika. Hata hivyo, hakuwataja marafiki hao lakini alikiri mwanaye kuhusishwa na mambo ya kishirikina.
Nakumbuka wakati ndoa yake na Hamad Ndikumana ikiingia kwenye mgogoro mzito na kuvunjika, Irene Uwoya alikaririwa akisema kuwa kuvurugika kwa mambo yake kulitokana na kulogwa na msanii mwenzake ambaye hakumtaja.
Huku nyuma, mastaa wa maigizo wa kitambo, Blandina Chagula ‘Johari’ na Nuru Nassor ‘Nora’ waliwahi kutamka wazi kuwa wanalogwa na wanawajua watu wanaowafanyia hivyo.
Nimetoa mifano hiyo michache kutoka kwenye Bongo Fleva na filamu lakini ukweli ni kwamba katika bendi za dansi nchini, hali ni mbaya zaidi. Kuna bendi ambayo hata uwalipe mabosi wake kiasi gani cha fedha hawawezi kukubali kufanya shoo katika ukumbi fulani kwa madai kuwa kuna bendi nyingine imefukia uchawi ukumbini hapo hivyo hawatapata watu.
Mifano hiyo inatupa picha halisi ya wasanii wetu kuwa hawaamini katika juhudi binafsi bali wanategemea nguvu za ndumba.
Baadhi yao wanajaribu kutafuta visingizo baada ya kuchuja kwenye gemu na muda wao kuwatupa mkono.
Wengine wameabudu bangi na madawa ya kulevya na katika kutafuta mchawi wakajikuta wakisingizia wamelogwa. Ipo mifano mingi. Jiulize nani anakuloga? Kwa nini anakuloga? Acheni kutafuta mchawi kwani kama wewe si mshirikina huwezi kuamini mambo ya kishirikina. For the love of game!

BI MWENDA APATA PIGO

Na Gladness Mallya
MSANII mkongwe kwenye filamu Bongo, Fatuma Makongoro ‘Bi Mwenda’ amepata pigo la kufiwa na mumewe anayejulikana kwa jina la Salum Mbegu.
Akizungumza kwa huzuni, Bi Mwenda alisema mumewe aliugua kwa muda mfupi ambapo Februari 14, mwaka huu alipelekwa katika Hospitali ya Amana ambapo aligundulika kuwa na tatizo la moyo kupanuka, akarudishwa nyumbani na siku iliyofuata (Februari 15) alifariki dunia.
Mipango ya mazishi ilitarajiwa kufanyika Jumamosi iliyopita nyumbani kwa marehemu, Kitunda, Dar. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.

STEVE ABANWA SKENDO YA KUTAFUNA RAMBIRAMBI, KUTOKA NJE YA NDOA

KAMA ilivyo kawaida ya safu hii, wiki iliyopita tulimweka kati mwigizaji wa filamu za Kibongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ambapo msomaji ulituma maswali yaliyohitaji majibu kutoka kwake, hapa anayajibu kwa ufasaha, SHUKA NAYO...

ELIMU
Nina furaha ya kuona kazi zako lakini pia napenda kufahamu elimu yako na mtazamo wako kwa jamii. Musa Lukwelo, Dodoma, 0712833104
STEVE NYERERE: Asante, nina elimu ya kidato cha nne, mtazamo wangu ni kuwasaidia Watanzania, hususan vijana wenzangu ili kuendeleza nchi yetu na kuongeza vipato vyao.
HISTORIA KWA UFUPI
Nakupongeza sana Steve kwa kazi nzuri, naomba kujua historia yako kwa ufupi, je, umeoa, una umri gani na una watoto wangapi? Mama Junior, Dar, 0717676615
STEVE NYERERE: Asante, nina mke na watoto wawili, Lisa na Alex, mengine ni siri yangu.
UBAGUZI
Kaka najua upo Bongo Movie Unity, sijui matarajio yenu mnataka muweje ila kwa muonekano wa nje mmejibagua wale mnaojiona mpo juu kuliko wenzenu, badilika kaka kumbuka mpanda ngazi hushuka, sipendi mashauzi yenu, nasikia una cheo pale! Cheo ni dhamana ndugu hukumbuki ulivyosota kabla? Kwa sasa jamii imeashaanza kuichoka kruu yenu, jichanganye na wale unaowaona si  lolote kwako. Baba Lily, Dodoma, 0717720023
STEVE NYERERE: Asante kwa ushauri wako nitaufanyia kazi.
KUCHAKACHUA RAMBIRAMBI
Nakupongeza kwa kazi nzuri ya kuielimisha jamii, hivi ni kweli huwa una tabia ya kuchakachua fedha za rambirambi? Gasto Luhunga, Tabora, 0754362412
STEVE NYERERE: Kila mtu anayefanya mazuri hategemei kulipwa mazuri zaidi ya kutukanwa na kudharauliwa.
KASOMEA KUIGIZA?
Hivi hiyo kazi uliisomea au kipaji tu? Dulla, Morogoro, 0654283038
STEVE NYERERE: Ni Mwenyezi Mungu amenijalia kipaji hiki, namshukuru.
MIGOGORO BONGO MOVIE
Hivi ni kweli Bongo Movie kuna migogoro, je, unafikiri chanzo ni nini? Elia, Iringa, 0718085308
STEVE NYERERE: Penye wengi hapakosi migongano na siku zote ili kitu kiimarike lazima migogoro iwepo.
KUTOKA NA UWOYA
Steve wewe ni bonge la staa katika tasnia ya filamu, eti ni kweli una uhusiano wa kimapenzi na (Irene) Uwoya? N. Man, Tanga, 0758900144
STEVE NYERERE: Hakuna kitu kama hicho.
USHAURI
Nafurahi sana kaka Steve kwa uigizaji wako maana unavaa uhalisia hasa ile filamu ya Baba Nyerere, nakuomba msiwe mnatoa filamu za mapenzi tu jaribuni kuigiza hata matukio ya jamii na kuwasaidia wasiojiweza. Mwaipopo, 0653317354
STEVE NYERERE: Nashukuru, asante sana.
NJE YA NDOA
Steve nawafahamu watoto wako wawili uliozaa nje ya ndoa, je, unawatunza? Cathy, Dar, 0758570870
STEVE NYERERE: Walete hao watoto kama unawajua.

KUIGA MAISHA YA RAY
Steven nakushauri usipende kujifanya maisha yako ni ya juu kwa kumuiga Ray (Vincent Kigosi), ishi kama ulivyo na usiwe kuwadi wa kuwatafutia mapedeshee wanawake, ipo siku watakugeukia wewe. Frank David, Dodoma, 0715360316
STEVE NYERERE: Asante.

MAYA: KUKUTANA NA LULU NI NGUMU

WASTARA, MAMA SAJUKI VISA VYAANZA

Stori:  Hamida Hassan na Gladness Mallya
IKIWA ni takribani siku siku 47 tangu alipofariki staa wa filamu za Kibongo, Juma Kilowoko ‘Sajuki’, kuna madai kuwa tayari visa vimeanza kati ya mkewe Wastara Juma na mama yake mzazi yaani mkwewe, Ijumaa Wikienda limetonywa.
Wastara Juma.
Kwa mujibu wa chanzo makini, mama Sajuki amekuwa akidaiwa kumfuatilia Wastara kwa kila anachokifanya hadi kufikia hatua ya kuwaambia watu wamchunguze.
Chanzo hicho kilidai kuwa Wastara na mama Sajuki walifikia hatua ya kurushiana maneno mbele za watu huku ulemavu wa mjane huyo wa Sajuki ukitajwatajwa.
“Unaambiwa wakija watu kumuombea dua Wastara na kumwambia atapata mwanaume mwingine, mama Sajuki anashindwa kuvumilia na kujikuta akiangua kilio,” kilidai chanzo hicho.

Mama mzazi wa Sajuki.
Kiliendelea kudai kuwa siku moja Wastara alitembelewa na watu kwenye ofisi yake iliyopo ndani ya nyumba anayoishi, Tabata-Bima, Dar ambapo mama Sajuki alidaiwa kuwafuatilia watu hao akitaka kujua mazungumzo waliyokuwa wakifanya na mkwewe huyo.
Kiliendelea kutiririsha madai kuwa siku ya arobaini ya Sajuki, mama Sajuki aliwaka mbele ya kadamnasi akikasirishwa na kitendo cha Wastara kupiga picha akidai huko ni kujitangaza.
HUYU HAPA WASTARA
Hata hivyo, ilidaiwa kuwa sakata hilo lilihamishiwa usiku kwani Wastara naye alikuja juu akiomba waweke kikao ili kuweka mambo sawa mbele ya baba Sajuki, mzee Juma Kilowoko.
Baada ya kujazwa habari hizo, dawati la Ijumaa Wikienda lilimtafuta Wastara ili kusikia upande wake juu ya ishu hiyo ambapo alisema kuwa pamoja na yote, kwa upande wake anamheshimu mama mkwe wake.
MAMA SAJUKI ALIKUWA NA HAYA
Alipotafutwa mama, alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli nilipata uchungu sana wakati wa arobaini kwani mama aliyekuwa akiendesha dua (Mariam Dedesi), alikuwa akisema tumuombee Wastara apate mwanaume mwingine, kama mzazi ni kweli nililia kwa uchungu na kutamka maneno mazito,” alisema mama Sajuki.